Posts

Showing posts from October 12, 2024

Mtoto wa kike apewe fursa ya kuongoza

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya mtoto wa kike Duniani, ambayo hufanyika kila mwaka Oktoba 11, jamii imeaswa kumshirikisha mtoto wa kike katika ngazi ya uongozi tangu anapoanza kukua mpaka anapokuwa mtu mzima. Hayo yalisemwa na Mkurugenzi wa taasisi ya Msichana Initiatives, Rebecca Gyumi alipokuwa akizungumza na wananchi wa Kata ya Lamaiti, Tarafa ya Mndemu, Wilaya ya Bahi, Mkoa wa Dodoma katika Tamasha la Msichana Amani Music Festival. “Siku hii katika nchi yetu, tunaongozwa na kaulimbiu ya Msichana na Uongozi, Mshirikishe Wakati ni Sasa. Kupitia jukwaa letu la Agenda ya Msichana, tumeitohoa zaidi kaulimbiu yetu ya kitaifa ambapo tunasema Msichana na uongozi, kwakutumia Fursa za Kidijitali au teknolojia ya kidijitali, kwa maana ya kuangalia namna wasichana wanavyoweza kuonesha uongozi kupitia fursa mbalimbali zinazopatikana kwenye teknolojia ya kidigitali” alisema Gyumi. Wakati akizungumza na kundi la wananchi na watoto wa kike alisema kuwa, ...

Sekunde chache kujiandikisha orodha ya wapiga kura

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Urahisi wa zoezi la kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura umekuwa kivutio kikubwa sana kwa wananchi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, kujitokeza na kushiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika ifikapo tarehe 27 Novemba, 2024. Wakazi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma waliojitokeza kushiriki zoezi hilo la uandikishaji wameeleza urahisi wake kuwa halichukui muda mrefu. Kwa upande wake Mariamu Paul, mkazi wa Mtaa wa Azimio, Kata ya Mpunguzi aliwashauri wananchi kujitokeza na kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura kwasababu zoezi halichukui muda mrefu. Aliongeza kuwa ni haki yao ya msingi na inawapa fursa kubwa ya kuchagua viongozi wa serikali ya mtaa wanaowataka na kuwaasa wasisubiri kuchaguliwa na watu wengine. “Nimekuja kujiandikisha na nawashauri wananchi wengine waje. Nimetumia kama sekunde kadaa tu kwa sababu hata haizidi dakika moja kuandikishwa na haichukui hata muda wako” alisisitiza Paul. Peter Agustino, mkazi wa Mtaa wa ...