Posts

Showing posts from April 20, 2024

Vipaumbele 13 vya mageuzi elimu msingi na sekondari 2024/2025

Image
OFISI ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwa mwaka 2024/25 imepanga kutumia shilingi trilioni 1.02 ili kutekeleza vipaumbele 13 kwenye sekta ya elimu vinavyolenga kusimamia na kuendesha elimu msingi na Sekondari. Akiwasilisha bungeni makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka huo, Waziri wa Nchi, TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa alisema fedha hizo zitajenga  vyumba vya madarasa 6,357, matundu ya vyoo 1,482, umaliziaji wa mabwalo 362 kati ya mabwalo hayo 15 ni msingi na 347 ni ya sekondari na umaliziaji mabweni 36 kwenye shule za awali na msingi. Pia alisema shule mpya 184, nyumba za walimu 184 na mabweni 186 katika shule za sekondari yatajengwa, sambamba na ununuzi wa vifaa vya TEHAMA kwenye shule za awali tatu, msingi 400 na shule za sekondari 500, ununuzi wa kemikali za maabara katika shule mpya 234. Mchengerwa alisema fedha hizo zitatumika katika utoaji wa ruzuku ya elimu bila ada kwa shule za msingi 17,986 na sekondari 4,894; ununuzi na usambazaji wa vita...

Watanzania watakiwa kupambana na rushwa na dawa za kulevya

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA WATANZANIA wametakiwa kushikamana na kupambana na rushwa, dawa za kulevya na uvunjifu wa haki za binadamu ili kujenga jamii iliyo bora. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora, George Simbachawene Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora, George Simbachawene alipokuwa akifungua mashindano ya mdahalo kwa shule za msingi, sekondari, vyuo vya kati na vyuo vikuu kuhusu madhara ya rushwa, matumizi ya dawa za kulevya, haki za binadamu na utawala bora katika ukumbi wa St. Gaspar Kisasa jijini Dodoma. Waziri Simbachawene alisema “baada ya watu kuwa wanashiba, elimu wanatapa kila kitu kinaenda vizuri, wanatazama televisheni wamepata ‘exposure’ mambo ni mazuri wameibuka maadui wengine. Maadui hao ni rushwa, dawa za kulevya na uvunjifu wa maadili na haki za binadamu, hao maadui watatu ni maadui wabaya sana, ni wajibu wa kila mmoja tushirikiane kupambana na maadui hao wa...