Posts

Showing posts from April 13, 2024

Shilingi Bilioni 1.5 kujenga Hospitali ya Wilaya Dodoma

Image
  Na. Dennis Gondwe, DODOMA SERIKALI imetoa shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Dodoma katika jitihada za kusogeza huduma bora za afya karibu zaidi na wananchi. Moja ya majengo ya Hospitali ya Wilaya ya Dodoma Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Andrew Method alipokuwa akiongelea mafanikio ya serikali ya awamu ya sita kwa kipindi cha miaka mitatu kwa waandishi wa habari ofisini kwake jijini hapa. Dkt. Method alisema “tunapoongelea mafanikio ya serikali ya awamu ya sita kwa kipindi cha miaka mitatu, mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa fedha shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Dodoma. Na hiyo hospitali ya wilaya ipo kimkakati kabisa, inajengwa eneo la Kata ya Nala. Ni eneo ambalo linaweza kufikiwa na rufaa ya vituo vyote vya afya ambavyo vinapitiwa na barabara ya mzunguko ‘ring road’. Kwa hiyo utaona hii barabara ya mzunguko inae...

Jiji la Dodoma lajenga vituo 8 vya Afya miaka 3 ya SSH

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeshuhudia ongezeko kubwa la ujenzi wa vituo vya afya nane katika serikali ya awamu ya sita inayolenga kuongeza miundombinu na kusogeza huduma za afya karibu na wananchi. Mkuu wa Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Andrew Method akielezea mafanikio ya divisheni yake Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Andrew Method alipokuwa akiongelea mafanikio ya miaka mitatu ya serikali ya awamu ya sita kwa waandishi wa habari ofisini kwake jijini hapa. “Ndugu waandishi wa habari, katika kipindi hiki cha miaka mitatu ya uongozi wa serikali ya awamu ya sita tumeshuhudia ongezeko kubwa la ujenzi wa vituo vya afya katika Jiji la Dodoma, tumejenga vituo vya afya nane. Mpaka sasa vituo viwili vimekamilika. Kituo cha Afya Chang’ombe kimekamilika. Mnafahamu eneo la Chang’ombe lina wakazi wengi zaidi ya 40,000 lakini hawakuwa n...