Posts

Showing posts from February 27, 2025

Maboresho ya elimu yapelekea kuongezeka kwa ufaulu katika Shule za Awali na Msingi Dodoma

Image
Na. Nancy Kivuyo, KIWANJA CHA NDEGE Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi Halmashauri ya Jiji la Dodoma yafafanua mafanikio ya maboresho ya elimu katika shule za msingi ambayo inafanya ufaulu wa wanafunzi kuongezeka. Ufafanuzi huo ulitolewa katika Mkutano wa Wadau wa Elimu na Utambulisho wa Mfuko wa Chakula na Lishe Shuleni ikiwa ni sehemu ya kujadili suala la lishe bora kuboreshwa kwa asilimia zote ili taaluma ya wanafunzi ifikie lengo tarajiwa. Akizungumza katika mkutano huo, Mkuu wa Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi, Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwl. Prisca Myalla alisema ā€œtunaishukuru serikali yetu kupitia Ofisi ya Rais ā€“ TAMISEMI kwa kuboresha elimu na kujenga miundombinu mizuri ambayo kwasasa inasaidia utoaji wa elimu kuwa mzuri. Katika suala la lishe, tunashukuru mfuko wa chakula na lishe shuleni kwasababu unasaidia wanafunzi kuhudhuria shuleni hali inayopelekea mahudhurio kuwa juu ukilinganisha na kipindi cha nyumaā€. Akizungumza kuhusu hali ya ufaulu na jumla ya s...

Matukio katika Picha ndani ya ukumbi wa Vijana katika Kikao cha Wadau wa Elimu Jiji la Dodoma

Image
 

Matukio katika Picha DC Shekimweri akikagua mabanda ya maonesho katika Siku ya Wadau wa Elimu Jiji la Dodoma

Image
Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri akitembelea mabanda ya maonesho kabla ya kuingia ukumbini kwa ajili ya Kikao cha Wadau wa Elimu Jiji la Dodoma na uzinduzi wa Mfuko wa Lishe shuleni uliofanyika katika ukumbi wa Vijana jijini Dodoma  

DC Shekimweri apongeza Jiji la Dodoma kupandisha ufaulu

Image
Na. Aisha Ibrahim, DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri, amewapongeza wadau na waratibu wa elimu kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kuhakikisha ufaulu wa wanafunzi ngazi ya msingi na sekondari unazidi kupanda kila siku katika Jiji la Dodoma. Alitoa pongezi hizo katika kikao cha wadau wa elimu na kuutambulisha mfuko wa lishe shuleni wa mwaka 2025, kilichofanyika ukumbi wa Vijana uliopo Kata ya Kiwanja cha Ndege, jijini Dodoma. Akizungumza katika kikao hicho alisema kuwa, lengo la Rais wa awamu ya sita, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuanzisha mpango wa lishe bora shuleni ni kukuza ufaulu wa wanafunzi na kuenzi kauli za Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, isemayo ā€œElimu tunayohitaji siyo tu ya kujua kusoma na kuandika bali ni elimu ya kujenga jamii yetu ya kufanya tuwe na uwezo wa kufanya kazi na kuleta maendeleo kwa wengineā€. Aliongeza kuwa, chini ya utawala wa Rais wa awamu ya sita, Dkt. Samia Suluhu Hassan, serikali imejitahidi kuboresha na kutekeleza kw...

Dodoma Jiji FC, mbioni kuwakabili Nyuki wa Tabora

Image
Na. Mussa Richard, TABORA Klabu ya Soka ya Dodoma Jiji FC, imewasili salama mkoani Tabora, ambapo mchana wa kesho watakuwa na kibarua cha kuikabili klabu ya soka Tabora United, (Nyuki wa Tabora) katika mchezo wa Ligi kuu ya NBC Tanzania bara, mchezo utakao vurumishwa majira ya saa 8 kamili mchana katika dimba la Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora. Akizungumza katika mkutano na waandishi wa Habari Kocha Mkuu wa Dodoma Jiji FC, Meck Mexime alisema ā€œMungu ametusaidia tumefika salama, maandalizi yote ya mchezo tulifanya tukiwa Dodoma, hapa tunakuja katika utekelezaji tu wa kile tulichokifanyia mazoezi, tunajua tunakuja kukutana na mpinzani mgumu. Lakini na sisi tumejiandaa katika mazingira yote kukabiliana nao, ukizingatia tunaelekea mwishoni mwa msimu. Kwahiyo, sisi kama Dodoma Jiji FC, tumejiandaa tuwe bora zaidi ili tuweze kupata matokeo mazuri na tuweze kuondoka na alama zote tatuā€. Nae, Augustine Nsata, ambaye ni Nahodha wa Klabu ya Soka ya Dodoma Jiji FC, akaweka wazi utayari wa k...

Diwani Makole asema neno kwa Machinga Dodoma

Image
Na. Shahanazi Subeti, MAKOLE Diwani wa kata ya Makole, Halmashauri ya Jiji la Dodoma Omary Haji amewapongeza wafanyabiashara wadogo wadogo (Machinga) wa Mkoa wa Dodoma kwa kuwa na umoja na mshikamano katika utendaji wa kazi kwa lengo la kujikwamua kiuchumi. Aliyasema hayo wakati wa makabidhiano rasmi ya Ofisi ya Viongozi wa Machinga Mkoa wa Dodoma iliyojengwa Kata ya Makole ambayo imegharimu shilingi milioni 56 zikiwa ni jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuona umuhimu wa Machinga katika taifa. Haji alisema ā€œnawashukuru sana Machinga wa Mkoa wa Dodoma, wakiongozwa na wenyeviti wao na viongozi wengine kwa kuweza kuungana katika kufanikisha ujenzi wa ofisi hii na kwakuwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ameweza kuwatambua Machinga wa Dodoma na kuwajengea ofisi katika eneo hili linaweza kuwasaidia na kuwarahisishia shughuli zenu za kibiashara. Kwahiyo, ni wazi kabisa mtalitunza na kulithamini vizuri jengo hiliā€. Sambamba na hilo alimpongeza Rai...

Dakika 5 kila Mkutano wa Baraza la Madiwani kupata dondoo za Afya Dodoma

Na. Dennis Gondwe, DODOMA Mkutano wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma umetenga dakika tano kwa ajili ya kupata elimu ya masuala mbalimbali ya Afya ili kuwajengea uelewa mpana madiwani. Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Mkutano wa Baraza la Madiwani, Prof. Davis Mwamfupe baada ya kuwasilishwa taarifa ya umuhimu wa siku ya Afya na Lishe ya Mtaa (SALIKI) katika mkutano wa Maraza la Madiwani uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Prof. Mwamfupe alisema alipendekeza kuwa kutokana na maelezo mazuri yaliyotolewa na Mkuu wa Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe kuhusu maana na umuhimu wa siku ya afya na lishe ya mtaa na lishe kwa ujumla kuna haja ya kutenga dakika tano katika kila mkutano wa baraza la madiwani kupata dondoo muhimu za afya. Awali akielezea maana ya Saliki, Mkuu wa Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe, Dkt. Sebastian Pima alisema kuwa Saliki ni siku ya afya na lishe ya mtaa. ā€œSiku hii ni mjumuisho wa hu...

Wananchi waaswa kujitokeza kwa wingi katika Kliniki ya Ardhi

Image
  Na. Aisha Ibrahim, VIWANDANI Afisa Maendeleo ya Jamii, Dawati la Msaada wa Kisheria Jiji la Dodoma, Frida Ngowi, amewataka wakazi wa jiji hilo kujitokeza kwa wingi katika Kliniki ya Ardhi inayoendelea kutolewa katika eneo la ilipokuwa Manispaa ya zamani kwa lengo la kupata msaada wa kisheria na kuweza kutambua njia muhimu za kutatua migogoro ya ardhi na kupata haki stahiki. Dawati hilo liko chini ya Kampeni ya 'Msaada wa Kisheria wa Mama Samia' ijulikanayo kama ā€œSamia Legal Aid Campaignā€ ambayo inaongozwa na Wizara ya Sheria na Katiba. Akizungumzia kuhusu msaada wa kisheria alisema kuwa lengo ni kuwasaidia wananchi wasiokuwa na uwezo wa kumudu gharama za Mahakama ili kuweza kutatua changamoto mbalimbali za Ardhi zanazohitaji msaada wa kisheria. ā€œLengo letu ni kutatua changamoto mbalimbali za watu wote wasioweza kupeleka madai yao mahakamani. Hivyo, sisi ni kiungo kati ya Mahakama na wananchi kupatiwa msaada wa sheriaā€ alisema Ngowi. Aliongeza kuwa, watu wote wana haki y...

DC Shekimweri apongeza Kliniki ya Ardhi jijini Dodoma

Image
Na. Aisha Ibrahim, VIWANDANI Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri, ameipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kurejesha tena Kliniki ya Ardhi inayolenga kutatua kero na changamoto mbalimbali za wananchi zinazohusiana na masuala ya Ardhi. Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri akisisitiza jambo Pongezi hizo alizitoa wakati wa ufunguzi wa zoezi la Kliniki ya Ardhi lililoanza leo na kuendelea mpaka tarehe 28 Februari, 2025, eneo la Halmashauri ya Manispaa ya zamani, jijini Dodoma. Akizungumzia kuhusu umuhimu wa kliniki hiyo, Alhaj Shekimweri alisema kuwa ni vema kufanya tathmini ya kero mbalimbali za Ardhi zilizopita na kuzitafutia ufumbuzi kabla ya kusikiliza kero mpya kwasababu itakuwa ni sawa na kufanya kazi bure kuzungumzia kero moja kila wakati. ā€œNi vema kufanya tathmini ya mazoezi yaliyopita kwasababu pengine kuna mtu zoezi lililopita alikuwepo na hili yupo kwa changamoto ile ile, huenda hajaridhika na huduma au majibu aliyoyapata kliniki iliyopita ndi...