Posts

Showing posts from January 6, 2025

Wafanyabiashara kuboresha huduma na kukuza biashara Mwaka 2025

Na. Halima Majid na Shahanazi Subeti, DODOMA Wafanyabiashara waweka wazi malengo ya kuboresha huduma ya kukuza biashara zao na kuchangia maendeleo ya uchumi ya Jiji la Dodoma mwaka 2025. Hayo yalisemwa na wafanyabiashara wa eneo la One Way lililopo katikati ya Jiji la Dodoma wakati wa mahojiano na waandishi wa habari walipokuwa wanaelezea salamu za jinsi walivyoupokea mwaka mpya 2025. Mfanyabiashara wa urembo, Luqman Olomi, katika Mtaa wa One Way alisema changamoto kubwa ni matatizo ya kifamilia yanayopelekea kurudishwa nyuma kiuchumi na kusababisha biashara yake kuyumba kwa kiasi flani. "Kuna changamoto za kifamilia zaidi ambazo huwa zinaturudisha nyuma kwa kiasi kikubwa kwa sababu inabidi utumie mpaka kiasi ambacho umeweka kwa ajili ya biashara na ili tufanikiwe inatakiwa tujitegemee na tusitegemee cha mtu. Hiyo ndio siri ya mafanikio na kwa anayoyafanya Rais wetu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa kushirikiana na mashirika mengi na taasisi mbalimbali anafanya vizuri” alis...

Viongozi Jukwaa la Wanawake Jiji la Dodoma wawezeshwa mafunzo

Image
Na. Coletha Charles, DODOMA Viongozi wa Jukwaa la Wanawake Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamewezeshwa mafunzo ya fursa za kiuchumi katika shughuli za biashara, kilimo, upatikanaji wa mitaji, sheria, ujasiriamali, matumizi ya teknolojia na mikopo ya asilimia kumi.   Mafunzo hayo yalifanyika katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Dodoma kwa lengo la kuwakutanisha wananawake ili waweze kujadili fursa na changamoto mbalimbali wanazokutana nazo wakati wa utekelezaji wa shughuli za kiuchumi.   Mwezeshaji wa mafunzo hayo, Kaimu Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Hidaya Mizega, aliwataka wanajukwaa hao kufahamu majukumu yao na sheria katika kuwezesha mafunzo kwa wanawake wengi kwa kufahamu masuala ya uchumi.   Alisema kuwa, viongozi hao wanajukumu katika mitaa na kata zao kuhamasisha shughuli za kiuchumi kwa kuibua miradi mikubwa na mizuri kupitia mikopo ya asilimia kumi ili kukuza ongezeko la uchumi kwa wanawake, kwa kufuata mwongozo mpya ambao um...