Posts

Showing posts from November 28, 2023

JIJI LA DODOMA KINARA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2023

Image
  Na. Dennis Gondwe, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imeibuka kinara katika mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2023 iliibuka nafasi ya kwanza kimkoa, kikanda na nafasi ya pili kitaifa. Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule (wa kwanza kushoto) akikabidhi cheti cha mshindi wa kwanza wa Mwenge wa Uhuru ngazi ya Mkoa na Kanda Jiji la Dodoma Taarifa hiyo ilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule alipokuwa akitoa maelezo mafupi kuhusu matokeo ya mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2023 katika kikao cha mkuu wa mkoa na wakuu wa wilaya na watendaji katika mkoa na halmashauri kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma. Senyamule alisema kuwa mwaka 2023 Mkoa wa Dodoma ulikuwa mkoa wa 30 kabla ya mkoa wa kilele kukimbiza Mwenge wa Uhuru. “Wakimbiza Mwenge wa Uhuru wanakuwa na vigezo wanavyoangalia hasa wanaangalia fedha zilizoletwa zimetumikaje, ubora wa miradi iliyoletewa fedha na Mheshimiwa Rais imesimamiwaje kwa tija na ufanisi kiasi gani...