Wilaya ya Dodoma kuchanja watoto zaidi ya laki 2 chanjo ya Polio
Na. Coletha Charles, NKUHUNGU Wilaya ya Dodoma imejipanga kuchanja watoto 207,096 chini ya miaka 10 dhidi ya ugonjwa wa Polio, sawa na asilimia 21 ya lengo la mkoa mzima, ikiwa ni utekelezaji wa kampeni ya kitaifa ya kujikinga na mlipuko wa ugonjwa huo. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo, iliyofanyika katika Shule ya Msingi Nkuhungu, Kata ya Nkuhungu Halmshauri ya Jiji la Dodoma Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri alisema kuwa wilaya hiyo imekamilisha maandalizi yote ya kimkakati kupitia vikao vya ngazi tatu wataalamu, makundi ya hamasa na Kamati ya Afya ya Msingi ya Wilaya. “Waliopewa kazi ya kuhamasisha, wafanye kazi hiyo ya uhamasishaji kikamilifu. Na kwa bahati njema, kama ambavyo tumeona hapa, wanatoka kwenye ngazi ya jamii, kwa hiyo wanafahamu namna ya kushirikiana na jamii. Tumepewa lengo la kuchanja watoto 207,096,” alisema Alhaj Shekimweri. Alitumia nafasi hiyo kubainisha kuwa nchi haina mgonjwa wa Polio kwa sasa, hatua hiyo ni maelekezo ...