Posts

Showing posts from August 28, 2026

Wilaya ya Dodoma kuchanja watoto zaidi ya laki 2 chanjo ya Polio

Image
Na. Coletha Charles, NKUHUNGU   Wilaya ya Dodoma imejipanga kuchanja watoto 207,096 chini ya miaka 10 dhidi ya ugonjwa wa Polio, sawa na asilimia 21 ya lengo la mkoa mzima, ikiwa ni utekelezaji wa kampeni ya kitaifa ya kujikinga na mlipuko wa ugonjwa huo. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo, iliyofanyika katika Shule ya Msingi Nkuhungu, Kata ya Nkuhungu Halmshauri ya Jiji la Dodoma Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri alisema kuwa wilaya hiyo imekamilisha maandalizi yote ya kimkakati kupitia vikao vya ngazi tatu wataalamu, makundi ya hamasa na Kamati ya Afya ya Msingi ya Wilaya. “Waliopewa kazi ya kuhamasisha, wafanye kazi hiyo ya uhamasishaji kikamilifu. Na kwa bahati njema, kama ambavyo tumeona hapa, wanatoka kwenye ngazi ya jamii, kwa hiyo wanafahamu namna ya kushirikiana na jamii. Tumepewa lengo la kuchanja watoto 207,096,” alisema Alhaj Shekimweri. Alitumia nafasi hiyo kubainisha kuwa nchi haina mgonjwa wa Polio kwa sasa, hatua hiyo ni maelekezo ...

Wilaya ya Dodoma kutumia vyombo vya habari katika kampeni ya dhidi ya chanjo ya Polio

Image
Na. Coletha Charles, NKUHUNGU Wilaya ya Dodoma imeweka mkakati wa kutumia vyombo vya habari, viongozi wa dini, shule na kampuni za simu ili kuwahamasisha wazazi kuwapeleka watoto kupata chanjo salama dhidi ya ugonjwa wa Polio, lengo likiwa ni kutokomeza kabisa hatari ya maambukizi ya ugonjwa huo. Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa zoezi hilo katika Shule ya Msingi Nkuhungu, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri, alisema kuwa vipindi vya redio na televisheni, hususani vipindi vya asubuhi, vitatumika kutoa elimu kwa wananchi na kujibu maswali kuhusu umuhimu na usalama wa chanjo hiyo. Alisema kuwa viongozi wa dini nao wamepewa nafasi muhimu katika uhamasishaji huo, kutokana na ushawishi wao katika jamii na uwepo wa watoto katika maeneo ya ibada, ikiwemo ‘Sunday Schools’, madrasa na jumuiya mbalimbali za kidini. “Tumeona pia kupitia eneo hilo kila mtoto wa Tanzania apate nafasi ya kupata chanjo hiyo. Tumewahamasisha shule zote, kamati na bodi za shule kufikisha ujumbe...