Posts

Showing posts from November 17, 2024

Chama cha AAFP chasifu mchakato wa uteuzi wagombea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Image
Na. Faraja Msibe, DODOMA CHAMA cha Alliance for African Farmers (AAFP) kimeridhishwa na mchakato wa uteuzi wa wagombea uliofanywa na wasimamizi wasaidizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma na kuuita kuwa ulikuwa shirikishi. Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Vijana wa Mkoa wa Dodoma wa Chama cha AAFP, Fredrick Mapua alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu mchakato wa uteuzi wa wagombea, mapingamizi na maamuzi ya rufaa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Mapua alisema “nimekuja kuzungumzia mchakato wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kuanzia uteuzi wa wagombea, mapingamizi na maamuzi ya rufaa. Nianze kwa kumshukuru sana Rais, mama Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri anayoendelea kuifanya amejaribu sana kusimamia demokrasia nchini. Mchakato ulienda vizuri sana. Tulifanya vikao baina ya wasimamizi wa uchaguzi na vyama vya siasa kwa ajili ya kufanya uchaguzi kuwa huru na wa haki. Hivyo, mchakato ulikuwa shirikishi tangu awali. Kwa chama chan...