Posts

Showing posts from August 30, 2023

WAZAZI MTAA WA MAZENGO WASHAURIWA KULEA WATOTO KATIKA MAADILI

Image
  Na. Dennis Gondwe, CHANG’OMBE WAZAZI wa Mtaa wa Mazengo Kata ya Chang’ombe wametakiwa kijikita katika malezi ya watoto ili wawe na maadili mema yatakayowawezesha kuwa raia wema na wawajibikaji katika jamii. Afisa Ustawi wa Jamii wa Kata ya Chang’ombe, Debora Kanuya Kauli hiyoilitolewa na Afisa Ustawi wa Jamii wa Kata ya Chang’ombe, Debora Kanuya alipokuwa akiongea na wananchi wa Mtaa Mazengo kwenye mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kufanyika katika Ofisi ya CCM Tawi la Chang’ombe Magharibi jijini Dodoma. Kanuya alisema “ninawaomba sana akina mama wa Mtaa wa Mazengo, tuwe na maneno mazuri kwa watoto wetu ili watoto wanapokuwa wawe wanafahamu maneno mazuri, wasiwe na maneno ya matusi na maneno ya mtaani. Lakini pia kuna baadhi ya akina mama ambao wamekuwa wakipiga sana watoto wao na kutoa lugha ya matusi. Unakuta baadhi ya kina mama wametelekezwa kwa hiyo zile hasira za kutelekezwa wanazihamishia kwa watoto, huo ni ukatili. Niwaombe sana wanawake...

MALEZI YA WATOTO YANAMCHANGO KATIKA USALAMA KATA YA CHANG’OMBE

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA AMANI na usalama wa Kata ya Chang’ombe inatokana na jinsi jamii inavyowalea watoto katika misingi bora na maadili mema. Kaimu Afisa Mtendaji wa Kata ya Chang’ombe, Daria Kapinga akiongea na wananchi Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Afisa Mtendaji wa Kata ya Chang’ombe, Daria Kapinga alipokuwa akiongea na wananchi wa Mtaa Mazengo kwenye mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Chama Cha Mapinduzi na kufanyika katika Ofisi ya CCM Tawi la Chang’ombe Magharibi. Kapinga alisema “ninatamani kuzungumza na mitaa miwili Mazengo pamoja na Msamalia suala la amani na ulinzi. Mitaa yetu imekuwa ni mitaa ambayo inatajwa sana kwenye sifa mbalimbali. Lakini chanzo nilichobaini ni kutoka kwenye mizizi ambapo ni kwa watoto wetu, kwenye malezi ya watoto wetu tumeshindwa kuidumisha amani, tumeshindwa kudumisha ulinzi kwa sababu ya malenzi tuliyonayo kwa watoto wetu. Malezi yasiyo mema kwa watoto matokeo yake ya muda mrefu yanapelekea kwenye uvunjifu wa amani na usalama”   ...

WANANCHI MAZENGO WATAKIWA KULEA WATOTO KATIKA MAADILI

Image
  Na. Dennis Gondwe, CHANG’OMBE JAMII imetakiwa kuwalea watoto katika maadili mema ili kuwa na taifa imara lenye watu wawajibikaji. Baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano wa hadhara Kauli hiyo ilitolewa na Katibu wa Hamasa na Chipukizi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Dodoma, Nasra Seif alipokuwa akiongea na wananchi wa Mtaa Mazengo kwenye mkutano wa hadhara ulioandaliwa na CCM na kufanyika katika Ofisi ya CCM Tawi la Chang’ombe Magharibi. Seif alisema “ndugu zangu tukiwalea watoto wetu katika maadili, tutakuwa na taifa ambalo ni imara lenye watu wanaowajibika ipasanyo. Siku hizi kumekuwa na tatizo kubwa sana la ukatili wa kijinsia kwa watoto. Twende tukawalee watoto kwa maadili na nidhamu. Kumbukeni alivyosema Afisa Mtendaji wetu wa Kata, Chang’ombe haitakuwa Chang’ombe ya matukio ya uhalifu, twende tukajifunze kutoka kwa wenzetu wa huko. Isionekane kama Chang’ombe ni sehemu ya watu ambao wameshindikana, hatutaki kuona ‘defender’ za Polisi zikipita Chang’ombe mara kw...