Posts

Showing posts from November 6, 2023

RAIS, DKT. SAMIA ATOA FIDIA YA BILIONI 4.5 KWA WAKAZI DODOMA

Image
Na. Queen Peter, DODOMA WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa amesema wananchi takribani 496 wa Jiji la Dodoma watapatiwa fidia ya kiasi cha Tsh. Bil. 4.5 ambazo tayari zimetolewa na Rais, Dkt. Rais, Dkt. Samia Suluhu ili   kulipa wananchi waliotwaliwa maeneo yao kwa ajili ya uendelezaji wa Jiji hilo. Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa (kushoto) akiongea na Waziri wa Madini, Anthony Mavunde (kulia) katika Kliniki ya Ardhi jijini Dodoma Waziri Silaa alisema hayo wakati wa zoezi la utatuzi wa migogoro ya Ardhi linaloendelea   katika uwanja wa Ofisi ya Ardhi Mkoa wa Dodoma alipofika hapo kwa lengo la kuongea na wananchi ikiwemo kukabidhi hati kwa baadhi ya wananchi. Waziri Silaa ameongeza kuwa wananchi watakao lipwa fidia hiyo ni wale ambao viwanja vyao vilitwaliwa kimakosa na kuzua malalamiko mengi hivyo hiyo ni hatua muhimu ya kutatua kero ya muda mrefu kwa wananchi hao. Aidha, aliwataka watumishi wa Wizara ya Ardhi, Nyumba...

WAZIRI SILAA APANIA KUMALIZA MIGOGORO YA ARDHI JIJI LA DODOMA

Image
  Na. Mwandishi wetu, DODOMA Waziri Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa amesema Wizara yake itahakikisha kero zote za migogoro ya ardhi zinakwisha katika Jijini la Dodoma ikiwa ni hatua muhimu ya utekelezaji   rasmi maagizo ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan. Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa akimsikiliza mwananchi katika Kliniki ya Ardhi Kata kwa Kata inayoendelea jijini Dodoma Akiongea na wananchi waliofika katika Kliniki ya Ardhi Waziri Silaa alisema kuwa lengo la kuweka kambi katika Ofisi ya Kamshina Msaidizi wa Ardhi wa Jiji la Dodoma ni kuhakikisha wanawahudumia wananchi ipasavyo. Waziri Silaa aliwaaambia wananchi waliofika kupata huduma katika kliniki hiyo kuwa atakuwa akifanya nao mazungumzo kila baada ya kumaliza ratiba ya bunge ili kujionea mwenyewe kero zinazowakabili wananchi hao. Mwananchi Foime Yohana alitoa dukuduku lake kwa Waziri Silaa baada ya kuwa na kero ya muda mrefu ya kuvamiwa na kuchukuliwa eneo lake n...

CD KAYOMBO AIPONGEZA TIMU YA SHIMISEMITA JIJI LA DODOMA KUZOA VIKOMBE 5 TAIFA

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA MKURUGENZI wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, John Kayombo ameipongeza timu ya watumishi wa jiji hilo iliyoshiki michezo ya Shirikisho la Michezo Serikali za Mitaa (Shimisemita) kitaifa kwa kuibuka mshindi wa jumla ikizoa jumla ya vikombe vitano. Mkurugenzi wa Jiji, John Kayombo akiinua juu kombe la ushindi wa jumla mashindano ya SHIMISEMITA. Kulia ni Mkuu wa Divisheni ya Utumishi na Rasilimali watu, Francis Kilawe akishuhudia tukio hilo Kayombo alisema hayo katika hafla fupi ya kukabidhiwa makombe ya Shimisemita katika ukumbi wa mikutano wa Jalmashauri ya Jiji la Dodoma. “Niseme machache, kwanza nawapongeza kwa hatua hii. Haya makombe matano siyo mchezo, kuna halmashauri zimekuja siku ya kwanza ya pili zikaondolewa. Mimi haya makombe matano ninatamba nayo mjini, maana yake kazi mliyofanya siyo ndogo, hongereni sana. Niwatie moyo mwakani tupo pamoja kwa utimamu zaidi” alisema Kayombo. Aidha, aliitaka timu ya mpira wa miguu ya watumishi wa Jiji la Dodoma...

TIMU YA WATUMISHI JIJI LA DODOMA YAIBUKA KIDEDEA KWA KUBEBA VIKOMBE 5 SHIMISEMITA TAIFA

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA TIMU ya Watumishi ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma iliyoshiriki michezo ya Shirikisho la Michezo Serikali za Mitaa (Shimisemita) ilikuwa tishio kwa kushinda michezo yote mpaka fainali na kuzoe vikombe vitano. Katibu wa Timu ya Watumishi Jiji la Dodoma, Emma Ernest alipokuwa akisoma taarifa fupi ya michezo ya Shimisemita Kauli hiyo ilitolewa na Katibu wa Timu ya Watumishi Jiji la Dodoma, Emma Ernest alipokuwa akisoma taarifa fupi ya michezo ya Shimisemita ngazi ya taifa mwaka 2023 kwa Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma katika hafla fupi ya kukabidhi vikombe walivyoshinda katika mashindano ya michezo ya Shimisemita katika ukumbi wa mikutano wa jiji hilo. Ernest alisema “katika michezo yote timu yetu ilikua ni tishio katika mashindano kwasababu michezo yote tuliyocheza hatukuwahi kufungwa hata mechi moja, tulishinda mechi zote kutoka hatua ya mzunguko mpaka fainali.   Timu ya mpira wa miguu ndiyo iliishia robo fainali kwa kutolewa na timu ya Halmashauri ya Wila...