Posts

Showing posts from July 22, 2023

AFISA MTENDAJI KATA YA CHAMWINO APEWA CHETI UTEKELEZAJI MKATABA WA LISHE JIJI LA DODOMA

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA AFISA Mtendaji wa Kata ya Chamwino, Lucas Nkelege amepongezwa na kupatiwa cheti kwa kufanya vizuri katika utekelezaji wa Mkataba wa Lishe katika jijini Dodoma. Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri akimkabidhi cheti kutambua kazi nzuri ya utekelezaji Mkataba wa Lishe Afisa Mtendaji Kata ya Chamwino, Lucas Nkelege Pongezi hizo zilitolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Lishe Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri alipoongoza Kikao cha Tathmini ya Mkataba wa Lishe kwa robo ya nne kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Shekimweri ambae ni Mkuu wa Wilaya ya Dodoma alisema kuwa suala la lishe ni muhimu kwa wilaya yake na maafisa watendaji wa kata wana wajibu wa kusimamia lishe katika maeneo yao. “Ndugu zangu, napenda kuwaambia tunatakiwa kuwa na tafsiri pana na dhamira ya Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhusiana na suala la lishe. Tuhakikishe watoto wanapata chakula shuleni. Wale wote amb...

JIJI LA DODOMA KUPELEKA TIMU YA MAAFISA MAZINGIRA NA AFYA KUKAGUA USAFI KATA YA IPAGALA

Image
Na. Dennis Gondwe, IPAGALA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma kupeleka timu ya maafisa mazingira na afya kufanya ukaguzi katika maeneo ya Mtaa wa Ipagala kukagua hali ya usafi wa mazingira kutokana na changamoto wa baadhi ya wakazi wa maeneo hayo kutojitokeza kufanya usafi wa mazingira. Mkuu wa Kitengo cha Usafi na uthibiti taka ngumu Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro akiongea na mamia ya wakazi wa Ipagala Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Kitengo cha Usafi na uthibiti wa taka ngumu Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro alipokuwa akiongea na mamia ya wakazi wa Kata ya Ipagala waliojitokeza katika usafi wa pamoja kwenye korongo la kitaa cheusi. Kimaro alisema “kwa sababu eneo hili lina changamoto ya wananchi kutojitokeza kufanya usafi katika maeneo yao. Wananchi wanalalamika kuwa watu wanaokaa kwenye nyumba zenye mageti hawajitokezi kufanya usafi na kuwaanchia wanaoishi katika nyumba zisizo na mageti kufanya usafi. Nimetoa maelekezo kwamba wiki ijayo kuanzia siku ya Jumatatu timu ya...