Posts

Showing posts from November 20, 2024

Rushwa Adui wa Haki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Image
Na. Coletha Charles, DODOMA Muelimishaji wa Darasa Tembezi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Chacha Marwa amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura ifikapo tarehe 27 Novemba, 2024 katika vituo husika.   Marwa alitoa elimu hiyo kwa wananchi waliopanda gari tembezi kutoka Soko la wazi la Machinga hadi Hospitali ya Benjamin Mkapa kwa kuwakumbusha kuwa haki ya kiongozi bora ipo mikononi mwao.   Alisisitiza kuwa kupiga kura ni msingi wa maendeleo katika mitaa yao kwa kuzingatia haki na kutokupokea rushwa ya aina yoyote kutoka kwa wagombea wa nafasi ya mwenyekiti na wajumbe watano (5) wa serikali za mitaa.   “Elimu hii ni muhimu kwa wananchi wote hasa mliojiandikisha kwenye orodha ya daftari la wapiga kura, ni muhimu sana kupata haki yako ya msingi, msipoenda kupiga kura mtashindwa kupata viongozi bora wa kuleta maendeleo. Mjitahidi kuchagua viongozi wazalendo wenye busara kwa kusikiliza sera zao. Pia walemavu ambao hawezi kufika katika vituo vya kupiga kura, s...

Kura Yako Maendeleo ya Mtaa

Image
Na. Coletha Charles, DODOMA Timu hamasa ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, imeendelea na zoezi la kuwahamasisha wananchi kushiriki kikamilifu katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika maeneo mbalimbali ya halmashauri hiyo.   Zoezi hilo lilifanyika katika eneo la Soko la wazi la Machinga hadi Ihumwa kwa lengo la kuwakumbusha na kuwasisitiza wananchi umuhimu wa kupiga kura kwasababu ni msingi mzuri wa kuleta maendeleo katika mitaa yao.   Muelimishaji wa katika gari maalum lijulikanalo kama darasa tembezi, Isabella Bruno alisema kuwa kupitia Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Dodoma kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, wametoa gari la darasa tembezi kwa lengo la kuhamasisha wananchi kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu.   Alisema kuwa wananchi wanatakiwa kuchagua viongozi wenye sifa kwa kusikiliza sera zao kipindi ambacho kampeni zitakapoanza tarehe 20 Novemba, 2024 na kuangalia kiongozi wa kuwaongoza kwa muda wa miaka mitano ya uongozi. ...

Jiji la Dodoma lasaini mkataba ujenzi wa barabara ya lami kwenda Hospitali ya Jiji

Image
Na. John Malima, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma imesaini mkataba wa makubaliano ya ujenzi wa barabara kutoka Hospitali ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma hadi barabara kuu ya Singida yenye urefu wa Kilomita 1.6 kwa kiwango cha lami. Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe (kustoto) na Mkurugenzi wa Jiji, Dkt. Frederick Sagamiko wakisaini mkataba wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami Mkataba huo ulisainiwa tarehe 20 Novemba, 2024 katika Ofisi ya Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma baina ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma na Kampuni ya ujenzi ya Kings Builders Limited ukiwa na thamani ya shilingi 2,431,050,561.63 (Bilioni Mbili na Milioni Mia Nne Thelathini na Moja Laki Tano na Mia Tatu Sitini na Moja na senti Sitini na Tatu). Katika zoezi la kusaini mkataba huo Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe alimshukuru Mkandarasi kwa kuunga juhudi za serikali na alimtaka kufanya kazi kwa viwango vinavyotakiwa. “Kwanza nawaponge...