Posts

Showing posts from March 6, 2024

Wanawake Dodoma watakiwa kujishughulisha

Image
Na. Dennis Gondwe, MSALATO WANAWAKE wametakiwa kujishughulisha na shughuli za uzalishaji mali ili kuweza kukuza kipato cha familia na taifa kwa ujumla kutokana na fursa za kazi zilizopo katika Mkoa wa Dodoma. Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Mkoa wa Dodoma, Mwl. Neema Majula akiongea na wanawake waliohudhuria Kliniki Zahanati ya Msalato Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Mkoa wa Dodoma, Mwl. Neema Majula alipokuwa akiongea na wanawake katika maadhimisho ya siku ya wanawake Kata ya Msalato yaliyofanyika katika Zahanati ya Msalato katika Kata ya Msalato. Mwl. Majula alisema kuwa kila mwanamke katika Mkoa wa Dodoma anatakiwa kujishughulisha ili kukuza kipato cha familia na taifa. “Ndugu zangu wakati mwingine ukatili wa kijinsia unatokana na kina mama kutokujishughulisha na uzalishaji mali katika ngazi ya familia. Hivyo, unyanyasaji unakuwepo kwa sababu kila kitu unamtegemea baba alete. Nata...

Msalato washauriwa kuwekeza kwenye Lishe ya watoto

Image
Na. Dennis Gondwe, MSALATO WAKAZI wa Kata ya Msalato wametakiwa kuwajenga watoto kiafya kwa kuwaandalia lishe bora ili kujenga taifa imara lenye uwezo wa kifikra na uchapaji kazi kwa ajili ya kuliletea maendeleo. Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Mkoa wa Dodoma, Mwl. Neema Majula Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Mkoa wa Dodoma, Mwl. Neema Majula alipokuwa akiongea wakazi wa Kata ya Msalato kwenye maadhimisho ya kuelekea siku ya wanawake duninia ngazi ya kata yaliyofanyika katika Zahanati ya Msalato iliyopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Mwl. Majula alisema “ndugu zangu hali ya lishe ni muhimu sana kwa watoto wetu. Tunapoanza kuwajenga watoto hawa wadogo wawe na lishe bora ndiyo tunajenga kizazi bora cha taifa hili. Tunakuwa tunawekeza kwenye afya na akili za watoto ambao baadae wanapoendelea kukua watakuwa wachapa kazi na wenye uwezo mzuri wa fikra na hivyo, kujiletea maendeleo yao na...

Msalato wamshukuru Rais, Dkt. Samia ujenzi wa shule

Image
Na. Dennis Gondwe, MSALATO WANANCHI wa Kata ya Msalato iliyopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamemshukuru Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwajengea shule mpya na kuwapunguzia wanafunzi kutembea umbali mrefu kufuata elimu. Afisa Mtendaji Kata ya Msalato, Devotha Selufara akimuelezea Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan alichoifanyia Kata ya Msalato Shukrani hizo zilitolewa na Afisa Mtendaji Kata ya Msalato, Devotha Selufara alipokuwa akiwatambulisha wataalam wa kata yake katika Shule ya Msingi Chikole kwa mgeni rasmi Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT) Mkoa wa Dodoma. Selufara alisema “Shule ya Msingi Chikole ina wanafunzi 790 ilianza mwaka jana mwezi Julai. Baada ya kumaliza ujenzi ulioanza mwezi Aprili, 2023 kwa fedha ya mama Samia Suluhu Hassan aliyotupatia shilingi 318,800,000 kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya ya msingi Chikole, ambapo tulijenga madarasa tisa, matundu 16 ya vyoo, jengo la utawala moja, tumefanikiwa kujenga madarasa ya chekechea ya mfano...