Posts

Showing posts from August 3, 2023

BANDA YA JIJI LA DODOMA LATOA TEKNOLOJIA UFUGAJI SAMAKI NA KUKU PAMOJA

Image
Na. Dennis Gondwe, NZUGUNI WANANCHI wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamehamasishwa kujifunza teknolojia ya ufugaji wa samaki na kuku kwa pamoja ili kujiongezea kipato. Afisa Uvuvi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Tausi Kiula Hamasa hiyo ilitolewa na Afisa Uvuvi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Tausi Kiula alipokuwa akihamasisha ufugaji wa pamoja wa samaki na kuku kwa wananchi waliotembelea banda la mifugo la Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Kiula alisema “tunawahamasisha wananchi wote waje wajifunze katika bwawa letu hapa. Kama unavyoona teknolojia nzuri ya kisasa ambayo unapoiona unahamasika. Unachimba bwawa la samaki kisha unajenga kibanda cha kuku kwa juu yake ili kuku wakiwa wanajisaidia kinyesi kinadondoka katika bwawa la samaki na kusaidia ‘fertilization’ kwa kuweka mbolea inayobadilisha maji kuwa ya kijani na kutengeneza chakula cha samaki”. Akiongelea umuhimu wa ufugaji huo alisema kuwa unawahakikishia samaki chakula bora. “Maji yanapobadilika kwenda rangi ya k...

WAFUGAJI KANDA YA KATI WASHAURIWA KULIMA MALISHO YA MIFUGO

Image
Na. Dennis Gondwe, NZUGUNI WAFUGAJI katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wameshauriwa kufanya ufugaji wa ndani na kulima malisho ya mifugo ili kujihakikishia kipato. Afisa Mifugo wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Anna Mchomvu Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Mifugo wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Anna Mchomvu alipokuwa akiongea na waandishi wa habari walipotembelea Banda la Mifugo la Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwenye maonesho ya Nanenane eneo la Nzuguni jijini Dodoma. Mchomvu alisema “tunahimiza wafugaji kufanya ufugaji wa ndani. Hivyo, ni muhimu mfugaji alime malisho yake kwa ajili ya kujiongezea kipato na tija ya maziwa na nyama. Wakati mwingine tunawafundisha ambao siyo wafugaji kulima malisho kama zao la biashara. Dodoma upatikanaji wa majani ni mgumu hivyo, mtu anaweza kulima malisho kama zao la biashara akayakata akayaanika na kuyafunga katika mfumo wa bezi na kuwauzia wafugaji. Na soko lipo wazi kabisa kwa wafugaji na bei ni nzuri beli moja tunalipata kwa shilingi 4,000-...

WAFUGAJI DODOMA WASHAURIWA KUFUGA NG'OMBE KISASA

Image
  Na. Dennis Gondwe, NZUGUNI WAFUGAJI katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wameshauriwa kufuga kisasa ng’ombe wachache wenye uwezo mkubwa wa kuzalisha. Amos Mwamyovellah, Mkurugenzi Mtendaji wa AJM&S Mwamyovellah Farm Production Kauli hiyo ilitolewa na Amos Mwamyovellah, Mkurugenzi Mtendaji wa AJM&S Mwamyovellah Farm Production alipokuwa akiongea na waandishi wa habari waliotembelea banda la mifugo la Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika maonesho ya Nanenane jijini Dodoma. Mwamyovellah alisema “ng’ombe hawa tumewaleta katika maonesho haya ya Nanenane ili kuwasaidia wenzetu wafugaji wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuweza kufuga kisasa. Wafugaji wanatakiwa kuwa na ng’ombe wa chache lakini wenye uwezo mkubwa kiuzalishaji”. Akiongelea chakula kinacholiwa na ng’ombe hao alisema kuwa wanakula chakula kizuri kilichoandaliwa kitaalam. “Chalula hiki kimechanganywa kitaalam kwa kutengeneza lishe bora kwa ng’ombe ili waweze kutupatia maziwa. Ng’ombe hawa tunakamua asubuhi, mc...