Vyama vya siasa vyapongezwa kudumisha Demokrasia jijini Dodoma
Na. Faraja Mbise, DODOMA Vyama vya siasa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma vimepongezwa kwa kuonesha ushirikiano mkubwa kuanzia mchakato wa uandikishaji wa orodha ya wapiga kura katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mpaka hatua ya kampeni za uchaguzi kwa wagombea mbalimbali. Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari pamoja na viongozi wa vyama vya siasa ofisini kwake Hayo yalisemwa na Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari pamoja na viongozi wa vyama vya siasa ofisini kwake. Dkt. Sagamiko alivipongeza vyama vya siasa kwa ushirikiano mkubwa waliouonesha katika michakato yote ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kuanzia kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura, kuchukua na kurejesha fomu za kugombea uongozi, pingamizi kuhusu uteuzi mpaka zoezi linaloendelea la kampeni za uchaguzi....