Posts

Showing posts from November 21, 2024

Vyama vya siasa vyapongezwa kudumisha Demokrasia jijini Dodoma

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Vyama vya siasa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma vimepongezwa kwa kuonesha ushirikiano mkubwa kuanzia mchakato wa uandikishaji wa orodha ya wapiga kura katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mpaka hatua ya kampeni za uchaguzi kwa wagombea mbalimbali. Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari pamoja na viongozi wa vyama vya siasa ofisini kwake Hayo yalisemwa na Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari pamoja na viongozi wa vyama vya siasa ofisini kwake. Dkt. Sagamiko alivipongeza vyama vya siasa kwa ushirikiano mkubwa waliouonesha katika michakato yote ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kuanzia kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura, kuchukua na kurejesha fomu za kugombea uongozi, pingamizi kuhusu uteuzi mpaka zoezi linaloendelea la kampeni za uchaguzi....

Vyama yatakiwa kufanya kampeni za kistaarabu Dodoma

Image
  Na. Dennis Gondwe, DODOMA VIONGOZI wa vyama vya siasa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kufanya kampeni za kistaarabu ili Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kufanyika kwa amani na utulivu. Msimamizi wa Uchaguzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko kiongea na waandishi wa habari na wadau wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Kauli hiyo ilitolewa na Msimamizi wa Uchaguzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipokuwa akiongea na waandishi wa habari na wadau wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ofisini kwake leo wakati akiwaelezea mwenendo wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Dkt. Sagamiko alisema kampeni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa mujibu wa Kalenda ya Uchaguzi zinafanyika siku saba kabla ya tarehe ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Hivyo, kampeni zilianza jana tarehe 20 Novemba, 2024 baada ya vyama vya siasa kuwasilisha ratiba ya mikutano ya kampeni kwa Msimamizi wa Uchaguzi. Ratiba hizo zilishawasilishwa kwa Mkuu wa Polisi Wila...