Shekimweri awapa maua yao Vijana Wilaya ya Dodoma
Na. Mussa Richard. DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Dodoma , Alhaj . Jabir Shekimweri amewapongeza v ijana walioshiriki katika Kongamano la Mwenge wa Uhuru la vijana 2025 lililofanyika katika u wanja w a Shule ya Msingi Mbwanga jijini Dodoma. Aliyasema hayo wakati akimkaribisha Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2025, Ndugu Ismail Ussi wakati wa kufunga Kongamano la Mwenge wa Uhuru la vijana. “Nimefarijika kuona vijana wamejitokeza kwa wingi na kushiriki ipasavyo katika mada mbalimbali ambazo zimewasi l ishwa na watoa mada pamoja na wachombeza mada . Pia n iwatoe wasiwasi vijana wote walioshiriki katika k ongamano hili kuwa mapendekezo yao nimeyapokea na nitayafanyia kazi ili kuhakikisha vijana katika Wilaya ya Dodoma wanajikwamua kimaisha kwa kutatuliwa kwa baadhi ya changamoto ambazo zinawakabi l i ” alisema Alhaj . Shekimweri. Katika hatua nyingine aliwapongeza watoa mada na wachombeza mada wote walioshiriki katika kutoa mada na mafunzo mbalimbali kwa vijana katik...