Posts

Showing posts from August 10, 2023

ASMA KARAMA ACHAGULIWA NAIBU MEYA JIJI LA DODOMA

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA ASMA Said Karama amechaguliwa kwa asilimia 100 kuwa Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika Mkutano wa Mwaka wa Baraza la Madiwani uliofanyika katika ukumbi wa halmashauri. Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Asma Said Karama Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo, Mwenyekiti wa Uchaguzi wa Naibu Meya, Sakina Mbugi alisema “Mheshimiwa Asma Said Karama amepata kura 55 sawa na asilimia 100 ya kura zote zilizopigwa na wajumbe. Kwa mamlaka niliyopewa ninamtangaza Mheshimiwa Asma Said Karama kuwa Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma”. Akitoa neno la shukrani Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Asma Karama alisema alimshukuru Mungu kwa baraka zake. “Napenda kukishukuru chama changu cha Mapinduzi kwa kuniruhusu kuingia kinyang’anyiro hiki. Kipekee zaidi napenda kuwashukuru madiwani kwa kuniamini na kunituma ili niwatumikie, tufanye kazi pamoja na kumsaidia Mstahiki Meya na kuwaletea maendeleo wana Dodoma. Kipekee zaidi nashukuru ...

MEYA AKEMEA UZALISHAJI MIGOGO JIJI LA DODOMA

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA MSTAHIKI Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe amekemea tabia ya uzalishaji migogoro ya ardhi na kusema inarudisha nyuma maendeleo ya halmashauri. Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe Prof. Mwamfupe alisema hayo alipokuwa akitoa muhtasari wa hoja zilizoibuliwa katika Mkutano wa Chama wa Mwaka wa Baraza la Madiwani uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Alisema “tunakemea watu wote wanaojihusisha na kuzalisha migogoro katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Na katika hili Mkurugenzi wa Jiji, watumishi wachukue nafasi zao na kwamba tutasimama kuhakikisha hatuibui migogoro mingine ya ardhi. Yapo maeneo madiwani wake wametuhumiwa kuhusika na migogoro ya ardhi. Rai ya kikao ilikuwa hawa wajitokeze tufanye nao mkutano wa Pamoja Meya, Mkurugenzi wa Jiji na Mkuu wa Divisheni ya Uendelezaji Makao Makuu. Mkutano huo ni wa kuwataka kutoa picha ya muelekeo wao na jinsi wanavyoifaham...

WAJUMBE WA KAMATI YA FEDHA JIJI LA DODOMA WATAKIWA KUJIHOJI

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA WAJUMBE wa Kamati ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kuhoji utendaji kazi wa halmashauri na kutoa ushauri utakaoifanya halmshauri hiyo kusonga mbele. Mwenyekiti wa Mkutano wa Mwaka wa Baraza la Madiwani, Prof. Davis Mwamfupe Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Mkutano wa Mwaka wa Baraza la Madiwani, Prof. Davis Mwamfupe baada ya kuunda Kamati ya Fedha na Utawala katika mkutano wa wazi uliofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji. Prof. Mwamfupe ambae ni Mstahiki Meya alisema kuwa Kamati ya Fedha na Utawala kwa mujibu wa kanuni itaongozwa na Mstahiki Meya. Wajumbe wake ni Mbunge Anthony Mavunde, Naibu Meya Asma Karama, Joan Mazanda, Daud Mkhandi, Jumanne Ngede, Bakari Fundikila, Ased Ndajilo, Grace Milinga, Neema Mwaluko na Elis Kitendya. “Yeyote aliyepangwa katika kamati hii atangulie kuamini kwamba ni imani yangu kwake, kwamba anaweza kufanya hivyo kuliko vinginevyo kwamba huyu alikuwa anataka hizi kamati siyo baraza...

JIJI LA DODOMA LAISHUKURU SERIKALI FEDHA ZA MAENDELEO

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imetoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha za kutekeleza miradi ya maendeleo kwa mwaka wa fedha 2022/2023 jambo lililosogeza huduma za kijamii na maendeleo karibu na wananchi. Mkuu wa Divisheni ya Mipango na Uratibu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Francis Kaunda Shukrani hizo zilitolewa na Mkuu wa Divisheni ya Mipango na Uratibu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Francis Kaunda alipokuwa akiwasilisha taarifa ya utendaji kazi na uwajibikaji wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kipindi cha mwaka 2022/2023 katika Mkutano wa Mwaka wa Baraza la Madiwani uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa jiji hilo. Kaunda alisema kuwa katika mwaka wa fedha ulioisha Halmashauri ya Jiji la Dodoma iliweza kutekeleza shughuli mbalimbali ikiwemo utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa ufanisi. “Kwa niaba ya Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma tunapenda kumshukuru Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa awa...