Posts

Showing posts from March 7, 2025

Wananchi 2,700 Kunufaika, Mradi wa Ukarabati Maji Taka

Na. Faraja Mbise, KIWANJA CHA NDEGE Takribani wakazi 2,700 wanatariwa kunufaika na mradi wa ukarabati wa mtandao wa maji taka unaotekelezwa na Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA) katika Mtaa wa Area C na D, Kata ya Kiwanja cha Ndege, jijini Dodoma. Hayo yalisemwa na Mhandisi wa Maji taka DUWASA, Mhandisi Yohana Koroso alipokuwa anawasilisha taarifa ya mradi wa ukarabati wa mtandao wa Maji taka katika eneo la Area C na D wakati wa ziara ya Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Dodoma. Mhandisi Koroso alisema ā€œmradi unagharimu jumla ya shilingi bilioni 4.9 ambao utawezesha jumla ya watu 2,700 kunufaika na mradi huo katika uondoaji wa Maji takaā€. Akizungumza wakati wa ziara ya Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Dodoma, alisema ukarabati wa miundombinu ya Maji taka una urefu wa Kilomita 19 za mabomba ya plastiki (PVC). Mhandisi Koroso alisema ā€œukarabati wa miundombinu ya maji taka maeneo ya Area C na D wenye urefu wa Kilom...

Bilioni 9.1 yanufaisha vikundi kwa Mwaka 2020-2023

Na. Faraja Mbise, IPAGALA Halmashauri ya Jiji la Dodoma ilitoa takribani ya shilingi bilioni 9.1 kwa ajili ya kuwezesha vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu ndani ya kipindi cha Mwaka 2020 hadi 2023. Hayo yalisemwa na Kaimu Afisa Maendeleo ya Jamii, Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Patrick Sebyiga alipofanyiwa mahojiano na waandishi wa habari, mara baada ya kumalizika kwa ziara ya Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Dodoma kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Jiji la Dodoma. ā€œKwa mikopo ya asilimia 10 kwa ajili ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, kuanzia Mwaka 2020 hadi 2023, Halmashauri ya Jiji la Dodoma imetoa kiasi cha shilingi bilioni 9.1 ikiwa na maana vikundi 767 vimepata mkopo. Vikundi vya akina mama 407, vijana 279 na watu wenye ulemavu 81 hii ni sawa na watu 4,883 wamenufaika na mkopo wa asilimia 10ā€ alisema Sebyiga. Akizungumzia kuhusu faida za mkopo wa asilimia 10, alisema kuwa mkopo huo una faida kubwa sana na unawawezesh...

Dodoma Queens yawakalisha Dodoma Jiji

Image
Na. Mussa Richard, DODOMA Klabu ya mpira wa kikapu ya wanawake ya Dodoma Queens imeibuka kidedea kwa kushinda vikapu 44 kwa 33 vya Dodoma jiji katika bonanza la kuelekea kilele cha Siku ya Wanawake Duniani Machi 8, mchezo uliopigwa katika viwanja vya Shule ya Sekondari Dodoma. Akizungumza baada ya mchezo huo, nahodha wa timu ya Dodoma Queens Respicia Mkulas alisema ā€œmchezo ulikuwa mzuri,na tumeweza kupata ushindi   wa tofauti ya seti 10, nitoe rai kwa wanawake wenzangu   kujitokeza kwa wingi kushiriki katika michezo mbalimbali kwasababu michezo ni afya, michezo ni burudani na pia michezo ni dawa inakukinga dhidi ya magonjwaā€. Nae, Jeni Kutawe, Nahodha wa timu ya kikapu ya Dodoma Jiji baada ya mchezo kutamatika akawaita wanawake kote nchini kushiriki kwenye mazoezi ili kuimarisha afya na kupunguza uwezekano wa kupata magonjwa. ā€œMchezo ulikuwa mzuri tumefurahi japo tumepoteza, mchezo huu ulikuwa siyo wa kushindana ulikuwa ni mchezo wa burudani kuhakikisha wote tunafurahi...

Dodoma Jiji FC, yawapigia hesabu kali Wanangushi

Image
Na. Mussa Richard, DODOMA Klabu ya Soka ya Dodoma Jiji FC, hii leo itashuka dimbani kukipiga na klabu ya Soka ya Coastal Union ikiwa ni muendelezo wa mbilinge mbilinge za duru ya lala salama ya ligi kuu ya NBC Tanzania Bara, mchezo utakaochezwa katika dimba la Jamhuri jijini Dodoma, majira ya saa 3 kamili usiku. Akizungumza wakati wa mkutano kabla ya mchezo, Kocha mkuu wa Dodoma Jiji FC, Meck Mexime aliweka wazi ugumu wa mchezo kuzingatia ligi inaelekea ukingoni. ā€œLigi inaelekea ukingoni mpaka sasa haijulikani nani anashuka nani anabaki jambo ambalo linafanya kila mchezo kuwa kama fainali. Kila timu tunayokutana nayo inakuwa imejiandaa vizuri lakini sisi hilo halitutishi kwasababu maandalizi yetu ni ya kufanya vizuri kwenye kila mchezo bila kujali ni nani tunaenda kukutana nae, jambo jingine linalofanya mchezo huu kuwa mgumu ni timu zote mbili tumetoka kupoteza michezo yetu iliyopita. Kwahiyo, kila timu inaingia kwenye mchezo huu kutafuta matokeo ili kuweza kutengeneza mazingira ma...

Mradi wa ujenzi Bweni Nala Sekondari unavutia

Image
Na. Nancy Kivuyo, NALA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma yatoa shilingi 25,000,000 kwa ajili ya umaliziaji wa ujenzi wa bweni la Shule ya Sekondari Nala kwa lengo la kuwaondolea wanafunzi kero ya kutembea umbali mrefu kwenda shule na kuongeza ufaulu. Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Afisa Elimu Sekondari Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwl. Fredrick Mwakisambwe alipokuwa akisoma taarifa ya umaliziaji wa bweni, vyoo na utengenezaji wa vitanda katika Shule ya Sekondari Nala kwa Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Dodoma. Mwl. Mwakisambwe alisema ā€œs hule hii ilianza rasmi tarehe 05 Aprili, 2005 ikiwa na wanafunzi 71 . Idadi ya wanafunzi iliendelea kuongezeka mwaka hadi mwaka na shule kukumbwa na changamoto mbalimbali , mojawapo ikiwa ni wanafunzi wengi kutembea umbali mrefu kutoka nyumbani. Hata hivyo , changamoto hi yo ilikuwa kubwa zaidi kwa wanafunzi wa kike na hivyo , uongozi wa shule pamoja na b odi waliomba kujengewa mabweni kwaajili ya wanafunzi wa kike kwa lengo la...

Mradi wa ukamilishaji Bweni Mbalawala Sekondari

Image
Na. Nancy Kivuyo, MBALAWALA Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Dodoma imefanya ziara katika Shule ya Sekondari Mbalawala kwa dhumuni la kukagua mradi wa ukamilishaji bweni ya wanafunzi kama moja ya miradi inayopaswa kukamilika na kutumika na wanafunzi wanaotoka maeneo ya mbali. Akisoma taarifa ya mradi wa ukamilishaji wa bweni la wasichana Shule ya Sekondari Mbalawala, Kaimu Afisa Elimu Sekondari Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwl. Fredrick Mwakisambwe alisema kuwa mradi ulianza kutekelezwa tarehe 14 Mei, 2009 chini ya usimamizi wa ofisi ya kata hadi hatua na upigaji plasta. ā€œIlipofika mwaka 2017 shule ilipokea kiasi cha shilingi 20,000,000 kutoka mapato ya ndani ya halmashauri kwa ajili shughuli za ukamilishaji wa kuondoa paa la zamani, k uongeza kozi moja ya tofa l i , k uweka dari ( g ypsum board) na k uweka mifumo ya umeme . K ujenga chumba cha matroni , k uskim u na kupaka rangi nje na ndani , k uchimba shimo la choo kwa ajili ya matundu manne na k ujenga bom...

Jiji la Dodoma latoa Mil. 20 kuchangia ufugaji Kuku

Image
Na. Faraja Mbise, IPAGALA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma ilikipatia mkopo usio na riba wa shilingi 20,000,000 Kikundi cha Winning Star kwa ajili ya kuongeza mtaji kwa shughuli ya ufugaji kuku wa mayai na nyama na kuongeza wigo wa ajira. Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Patrick Sebyiga wakati akisoma taarifa ya Kikundi cha Winning Star kinachojishughulisha na ufugaji wa kuku wa mayai na nyama katika Kata ya Ipagala mbele ya kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Dodoma ilitotembelea kikundi hicho. Sebyiga alisema ā€œl engo kuu la kikundi hiki ni kutumia fursa ya ufugaji ili kuajiri na kutoa ajira kwa wengine hasa vijana . Ai dha , kujikwamua kiuchumi kwa sababu kwa kufanya hivyo , kikundi kimeondoa u tegemezi na umasiki kwenye familia hupungua. Matamanio ya kikundi ni kufuga kuku 10,000 kutokana na uhitaji mkubwa wa mayai hapa Dodoma ā€ . Akiongelea mtaji wa kikundi hicho, Kaimu Afisa Maendeleo ya Jamii Jiji huyo...

Ofisi Mpya ya DC Dodoma kuboresha utoaji huduma

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA MAKULU Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Dodoma yamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha kwa ajili ya kujenga Ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Dodoma ambayo italeta tija ya kuwahudumia wananchi wote wa Mkoa wa Dodoma. Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Dodoma kwa Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Afisa Tawala katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Merina Ijiko alisema kuwa utekelezaji wa mradi huo umekamilika na upo katika hatua ya kipindi cha uangalizi cha mwaka mmoja ambacho kilianza tarehe 10 Juni, 2024 na kuisha tarehe 9 Juni, 2025. Akiongelea fedha za mradi huo, alisema kuwa j umla ya shilingi 1,242,969,735.30 zimelipwa kwa m kandarasi ikiwa ni asilimia 61.89 ya g harama za mradi hadi sasa. Mkandarasi anadai jumla ya shilingi 5 7 8 , 288 ,9 69 .19 na mhandisi mshauri ameshalipwa jumla ya shilingi 68,380,000.00 ikiwa ni malipo ya marejeo y...

Halmashauri ya Jiji la Dodoma yatoa Kongole kwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan

Image
Na. Faraja Mbise, NZUGUNI Halmashauri ya Jiji la Dodoma inaendelea kutoa shukrani kwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutenga fedha kwa ajili ya maboresho ya miundombinu ya sekta ya afya kwa kipindi chote cha miaka minne ya uongozi wa awamu ya sita inayopelekea huduma bora kwa wananchi. Hayo yalizemwa na Mganga Mkuu wa Jiji la Dodoma, Dkt. Sebastian Pima wakati akiwasilisha taarifa fupi ya Zahanati ya Mahomanyika kwa Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Dodoma iliyofanya ziara ya kutembelea zahanati hiyo. Dkt. Pima alisema ā€œtunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutenga fedha kwa ajili maboresho ya miundombinu ya sekta ya afyaā€. Akizungumza kuhusu historia ya zahanati hiyo, alisema kuwa mwaka ambao zahanati hiyo imejengwa na jumla ya watumishi waliopo wanaowahudumia wananchi wa Mtaa wa Mahomanyika. ā€œZahanati ya Mahomanyika ilianzishwa mwaka 1992 na inapatikana katika Kata ya Nzuguni. Zahanati hii ina jumla y...