Ufugaji wa Ng'ombe aina ya Friesian njia bora ya kuongeza kipato
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Wananchi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamehimizwa kuwekeza katika ufugaji wa ng ’ ombe wa maziwa aina ya Friesian kama njia ya kuongeza kipato, kuimarisha usalama wa chakula na kuinua uchumi wa familia kupitia uzalishaji wa maziwa. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Dkt. John Malecela (Nzuguni), Afisa Mifugo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Frank Mosses alisema kuwa ng ’ ombe aina ya Friesian ni miongoni mwa mifugo yenye tija kubwa kutokana na uwezo wake wa kuzalisha maziwa kwa wingi endapo atatunzwa kwa lishe bora, maji ya kutosha na usimamizi sahihi. “ Tunatoa elimu kwa wananchi kuhusu ufugaji bora wa ng ’ ombe wa maziwa aina ya Friesian, hususan namna ya kuwapatia lishe sahihi, chanjo, maji safi na mazingira bora ya kuishi ili kuongeza uzalishaji wa maziwa. Lengo ni kuwasaidia wafugaji kupata tija na kuboresha maisha yao kupitia ufugaji wenye ufanisi na watija, ” alisema Mosses. Kwa upande ...