Posts

Showing posts from October 7, 2024

Mkoa wa Dodoma kinara Mazingira ya Uwekezaji

Image
Na. Asteria Frank, DODOMA Mkoa wa Dodoma umeibuka kinara kwa kuwa mkoa wa kwanza kupokea tuzo za uwekezeji na utengenezaji wa mazingira wezeshaji ya biashara kutoka kwa Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Biashara, Dkt. Samia Suluhu Hassan. Tuzo hiyo imekabidhiwa na Mwenyekiti wa “Chember of Commerce” (TCCIA) kwa Mkuu wa Mkoa Dodoma, Rosemary Senyamule katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa niaba ya Dkt. Samia Suluhu Hassan tarehe 7 Oktoba, 2024. Senyemale alisema kuwa kupokea tuzo hiyo ni heshima kubwa sana na inahamasisha namna ya kuendelea kuboresha mazingira wezeshaji ya biashara kila siku. “Sisi kwa Mkoa wa Dododma tunajua tunazo fursa nyingi lakini pia tunao wafanyabiashara wengi kwa vitengo mbalimbali na tunashukuru kuwa tuzo hizi tunazipata sio kwa Serikali ya Mkoa kusema sisi tunafanya vizuri, Tuzo hizi zinatolewa baada ya wafanyabiashara wenyewe kusema tunaonaje huduma tunazo zipata kutoka serikalini” alisema Senyamule. Aidha, Mwenyekiti wa TCCIA Dodoma, Vivian Komu, alitoa ta...

KADI YA MPIGA KURA SIO LAZIMA KWENYE UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri, amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika zoezi la kujiandikisha kwenye orodha ya mpiga kura zoezi litakalofanyika kwa muda wa siku kumi kuanzia tarehe 11- 20 Oktoba, 2024 na kusema kuwa kadi ya mpiga kura siyo kigezo cha kupigia kura. Mkuu wa Wilaya ya Dodoma alisema hayo alipokuwa akizungumza na mamia ya watumishi wa umma na wananchi waliojitokeza katika Bonanza la kuhamasisha umma kujitokeza katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika Shule ya Sekondari Dodoma iliyopo Mtaa wa National Housing, Kata ya Makole jijini Dodoma. Alhaj Shekimweri alisema “hakuna kadi ya mpiga kura kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, siku ya kupiga kura unaweza kwenda na kitambulisho chochote kile kama leseni ya udereva, kadi ya mpiga kura ya uchaguzi mkuu, kadi ya bima ilimradi utambulishwe na kadi yoyote. Na kama hauna kabisa basi hata jirani yako anaeaminika kuwa ni mkazi na ana kadi husika anaweza kukutambulisha”. ...