Posts

Showing posts from November 1, 2023

RAIS, DKT SAMIA ATOA BIL 4.5 KULIPA FIDIA WANANCHI DODOMA

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA RAIS, Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa shilingi bilioni 4.5 kwa ajili ya kulipa fidia wananchi 469 wa maeneo mbalimbali katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, John Kayombo alipokuwa akiongelea mafanikio ya serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Uzinduzi wa Mikutano ya Wakuu wa Mikoa na Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa na Waandishi wa Habari katika kampeni ya Tumekusikia Tumekufikia uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma. Kayombo alisema “Mheshimiwa Rais kwa upendo wake ameleta fedha shilingi bilioni 4.5 kwa ajili ya kuwalipa fidia wananchi waliochukuliwa maeneo yao kwa ajili ya shughuli mbalimbali. Jumla ya wananchi 469 wanatarajia kulipwa kuanzia sasa, fedha tumezipokea tayari”. Akiongelea changamoto ya ‘double allocation’, alisema kuwa Rais alielekeza wananchi hao wa...

SERIKALI YATOA BIL 1 UJENZI HOSPITALI YA WILAYA DODOMA

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA SERIKALI imetoa shilingi bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Dodoma kwa lengo la kuboresha huduma za afya na kuzisogeza huduma hizo karibu zaidi na wananchi. Mkurugenzi wa Jiji, John Kayombo akiongea na waandishi wa habari Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, John Kayombo alipokuwa akiongelea mafanikio ya serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Uzinduzi wa Mikutano ya Wakuu wa Mikoa na Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa na Waandishi wa Habari katika kampeni ya Tumekusikia Tumekufikia uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma. Kayombo alisema “kwa upande wa afya mheshimiwa rais ameleta fedha nyingi. Ameleta shilingi bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Dodoma inayojengwa eneo la Nala. Kituo cha Afya Makole kimekuwa kikipokea watu wengi sana, mheshimiwa Rais ametuletea shilingi milioni 750 kwa ajili...

JIJI LA DODOMA LAPOKEA ZAIDI YA BIL 5 SEKTA YA ELIMU MSINGI

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imepokea zaidi ya shilingi bilioni tano kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya elimu ya msingi kutoka kwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya kuboresha sekta ya elimu. Mkurugenzi wa Jiji, John Kayombo Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, John Kayombo alipokuwa akiongelea mafanikio ya serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Uzinduzi wa Mikutano ya Wakuu wa Mikoa na Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa na Waandishi wa Habari katika kampeni ya Tumekusikia Tumekufikia uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma. Kayombo alisema “kwa upande wa elimu ya msingi, tumepokea zaidi ya shilingi bilioni tano kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya elimu ya msingi. Tumepokea shilingi bilioni tatu kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya tatu ambazo ujenzi unaendelea”. Awali akifungua mkutano huo, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknol...

RAIS DKT. SAMIA ATOA FEDHA KIBAO KUTEKELEZA MIRADI JIJI LA DODOMA

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa fedha nyingi kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo kwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa lengo la kuboresha maisha ya watanzania. Mkurugenzi wa Jiji, John Kayombo akiongea na waandishi wa habari Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, John Kayombo alipokuwa akiongelea mafanikio ya serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Uzinduzi wa Mikutano ya Wakuu wa Mikoa na Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa na Waandishi wa Habari katika kampeni ya Tumekusikia Tumekufikia uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma. Kayombo alisema “Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya mambo makubwa kwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika sekta ya elimu sekondari. Mheshimiwa Rais ametuletea shilingi 260,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni mawili katika Shule ya Sekondari ya wasich...