Posts

Showing posts from August 13, 2024

Kata ya Zuzu yajivunia mafanikio ya utekelezaji miradi ya maendeleo

Image
Na. Valeria Adam, DODOMA SERIKALI yapongezwa kwa utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayolenga kuboresha maisha ya wananchi wa Kata ya Zuzu ikiwa na matokeo chanya. Diwani wa Kata ya Zuzu, Awadh Abdallah Pongezi hizo zilitolewa na Diwani wa Kata ya Zuzu, Awadh Abdallah nje ya ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Diwani Abdallah alisema kuwa miradi ya ujenzi wa madarasa mapya, visima vya maji na barabara za lami inakwenda sambamba na malengo ya serikali ya kuhakikisha huduma bora kwa wananchi. Miradi hiyo imeanza kutoa matokeo chanya na wananchi wanaendelea kunufaika nayo. "Kwanza tunatekeleza mradi mkubwa wa Kituo cha Afya Zuzu kitakachogharimu shilingi milioni 550 na mpaka sasa takribani shilingi millioni 320 tumeshazipokea na ujenzi unaendelea. Tumejenga madarasa nane, matundu 16 ya vyoo na ofisi za walimu kwa ajili ya kidato cha tano na sita ambao tunatarajia mwaka unaofuatia tutaanza kuwa na wanafunzi wa kidato cha tano na sita. "Lakini pia tunaj...

Diwani Chibago azindua zoezi la ugawaji baiskeli 150 kwa wanafunzi wa Jiji la Dodoma

Image
Na.   Flora    Nadoo, MPUNGUZI Mwakilishi wa Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Fadhil Chibago amezindua zoezi la ugawaji wa baiskeli 150 kwa wanafunzi wa kike na kiume wanaotembea umbali mrefu kufuata elimu. Chibago ambae ni Diwani wa Kata ya Dodoma Makulu alizindua zoezi hilo katika Shule ya Sekondari Mpunguzi iliyopo jijini Dodoma. Mwakilishi wa Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Fadhil Chibago akimkabidhi mmoja wa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mpunguzi baiskeli Diwani Chibago alisema “zoezi hili linahusisha ugawaji wa baiskeli 150 katika shule tano za sekondari za Mkoa wa Dodoma. Baiskeli hizi ili ziishi ni lazima sisi tuzitunze. Hivi si vyombo ambavyo ni kamili, haviwezi kuharibika, vitaharibika. Lakini je ni sahihi kwamba baiskeli ikiwa imepata pancha irudishwe? Jibu ni hapana, kwa sababu hii haijakaa sawa, yale matatizo madogo madogo tunaweza kuyatatua wenyewe. Hivyo, basi kuna msemo unaosema kuwa ukibebwa na wewe bebeka. Shirika h...