Posts

Showing posts from April 12, 2025

Zabibu Hoteli Dodoma yajikita matumizi ya Nishati safi

Image
Na. Mussa Richard, TAMBUKARELI Kampeni ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuhakikisha taasisi na sehemu zenye mkusanyiko wa watu zaidi ya 100 kutumia nishati safi ya kupikia, imepokelewa na kufanyiwa kazi ipasavyo na uongozi wa Zabibu Hoteli, iliyopo Kata ya Tambukareli jijini Dodoma. Hayo yamebainishwa na Meneja Mkuu wa Zabibu Hoteli, Mathew Gabriel, wakati akizungumza na vyombo vya Habari baada ya kutembelea hoteli hiyo ili kujionea matumizi ya nishati safi katika hoteli hiyo. ā€œZabibu Hoteli ni miongoni mwa taasisi ambayo imejizatiti kwenye matumizi ya nishati safi ya kupikia kwenye kila nyanja inayohusu mapishi. Nishati safi ya kupikia ni nzuri na ina faida nyingi kulinganisha na nishati zingine zinazochangia kwenye uchafuzi wa mazingira. Kwahiyo, niziombe sekta zote na watu binafsi wajikite katika matumizi ya nishati safi za kupikia kwasababu ni rahisi na salamaā€ alisema Gabriel. Nae, Focus Mwenda, Mpishi Mkuu wa Zabibu Hoteli, alimshukur...

Wananchi Tambukareli wafurahia barabara miaka minne ya Rais Samia

Image
Na. Mussa Richard, TAMBUKARELI Diwani wa Kata ya Tambukareli jijini Dodoma, Juma Michael, amesema kuwa ndani ya miaka minne ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amejenga barabara ya kiwango cha lami inayoanzia ā€˜ Shoppersā€™ hadi Kituo Kikuu cha Mabasi Dodoma kwa lengo la kupunguza msongamano na kurahisisha huduma ya usafiri. Diwani Michael, alisema hayo baada ya kutembelewa na waandishi wa habari ofisini kwake kwa lengo la kujionea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa kwenye Kata ya Tambukareli kwa kipindi cha miaka minne ya uongozi wa awamu ya sita chini ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan. ā€œKipindi cha nyuma tulikuwa na changamoto ya barabara, lakini tunaishukuru sana serikali imeweza kusikia kilio chetu na kuweza kutujengea barabara yenye kiwango cha lami. Barabara ambayo imekuja kuwa mkombozi kwa wafanyabiashara, wajasiriamali na wananchi kwa ujumla, kwasababu hapo awali wafanyabiashara walikuwa wana shindwa jinsi ya kufikisha bidhaa katika ...