Posts

Showing posts from February 13, 2024

Wazazi Chamwino washauriwa kutenga muda kuzungumza na watoto

Image
  Na. Dennis Gondwe, CHAMWINO WAZAZI na walezi katika Wilaya ya Dodoma wameshauriwa kutenga muda wa kukaa na kuongea na watoto wao ili waweze kubaini changamoto zinazowakabili ikiwemo kufanyiwa vitendo vya ukatili wa kijinsia. Cpl. Edith Siwango kutoka Dawati la Jinsia na Watoto wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Dodoma alipokuwa akiongea na wanafunzi, walimu na wadau wa Lishe katika Shule ya Msingi Chamwino Ushauri huo ulitolewa na Cpl. Edith Siwango kutoka Dawati la Jinsia na Watoto wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Dodoma alipokuwa akiongea na wanafunzi, walimu na wadau wa masuala ya Lishe katika Shule ya Msingi Chamwino iliyopo Kata ya Chamwino Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Cpl. Siwango alisema “tupo hapa kwa ajili ya kuwalinda watoto wetu. Wazazi na walezi mlio hapa nawaomba mtenge muda wa kuzungumza na watoto wenu. Mazungumzo hayo yatawasaidia kuwaelewa watoto wenu. Watoto wamekuwa wakipitia changamoto mbalimbali zinazohusisha ukatili wa kijinsia na kushindwa kuwaeleza wazazi na ...

MAMIA WAJITOKEZA KUMUAGA LOWASA KARIMJEE, WAKO PIA VIONGOZI WA DINI

Image
  MAMIA ya watu wamejitokeza katika Viwanja vya Karimejee jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kuuaga mwili wa aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, huku zoezi hilo likitarajiwa kuongozwa na Makamu wa Rais, Dkt. Phillip Mpango. Leo Jumanne, Februari 12, 2024, mwili wa Lowassa unatarajiwa kuagwa katika Viwanja hivyo ambapo viongozi mbalimbali wa kiserikali akiwemo Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mawaziri wengine wamehudhuria. Mbali na mawaziri wa Tanzania Bara, Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Makamu wa kwanza wa Rais Zanzibar, Othman Masoud Othman na mawaziri kadhaa wa visiwa hivyo, wamehudhuria kwa ajili ya kushiriki hafla hiyo ya mwisho kwa Lowasa. Viongozi wengine wa vyama vya siasa akiwemo Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika na viongozi wa dini, wamehudhuria shughuli hiyo. Jeneza lililobeba mwili wa Lowassa huku likiwa limefunikwa na bendera ya Tanzania, limeingia uwanjani hapo majira ya 10.20. Shughuli hiyo inatanguliwa na ibada fupi inayoongozwa...

Matukio katika picha mazoezi kwa afya na uhamasishaji Lishe Shule ya Msingi Chamwino

Image
 

PUMZIKA KWA AMANI MHESHIMIWA EDWARD LOWASSA

Image
 

Wanafunzi Chamwino wahimizwa kula mboga za majani

Image
Na. Dennis Gondwe, CHAMWINO WANAFUNZI wa Shule ya Msingi Chamwino wametakiwa kula kwa wingi mboga za majani ili kuwa na lishe bora itakayowasaidia kusanya vizuri katika masomo yao. Afisa Lishe kutoka Kituo cha Afya Makole, Ezeleda Mongo (mwenye tisheti nyeupe) akiwafundisha wanafunzi jinsi ya kusia mbegu Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Lishe kutoka Kituo cha Afya Makole, Ezeleda Mongo alipokuwa akiongea na wanafunzi, walimu na wadau wa lishe katika tukio za kusia mbegu za mboga za majani katika Shule ya Msingi Chamwino. “ Nimefurahi kujumuika nanyi katika hili zoezi la kuhamasisha mazoezi na zoezi la upandaji wa mbogamboga. Ninashauri sana jamii itumie mbogamboga na matunda zaidi kwa ajili ya kuhamasisha afya. Magonjwa yasiyo ambukiza yanaweza kutibika kwa njia ya chakula hususani mbogamboga na matunda” alisema Mongo. Aidha, aliwashauri wanafunzi kuwa wanakula mbogamboga kwa wingi. “Wito wangu hata kwa watoto wa shule wanapokuwa wanaendelea kukua wale mbogamboga za majani kwa win...

Kata ya Chamwino kipaumbele Lishe shuleni

Image
  Na. Dennis Gondwe, CHAMWINO KATA ya Chamwino imetoa kupaumbele katika agenda ya lishe ili kuhakikisha wanafunzi wanakuwa na lishe bora na kuendelea na masomo yao vizuri. Afisa Mtendaji wa Kata ya Chamwino, Lucas Nkelege akiongelea umuhimu wa Lishe shuleni Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Mtendaji wa Kata ya Chamwino, Lucas Nkelege alipokuwa akiongea na walimu, wanafunzi na wadau wa masuala ya lishe katika Shule ya Msingi Chamwino iliyopo katika Kata ya Chamwino, Halmashauri ya Jiji la Dodoma. “Leo ni maadhimisho ya kidunia kuhamaisha matumizi ya mimea jamii ya mikunde. Kama maharage, njegere, choroko, mbaazi. Sisi Kata ya Chamwino suala la lishe lina umuhimu mkubwa sana. Lengo ni kupinga hali ya udumavu, ukondefu na athari zote zinazotokana na lishe duni. Kata ya Chamwino tumeweka mikakati mizuri kuhakikisha wanafunzi katika shule zetu tatu za msingi na moja ya sekondari wanaweza kupata chakula shuleni. Na leo hapa tumekuja Shule ya Msingi Chamwino yenye wanafunzi takribani ...

Wanafunzi Dodoma watakiwa kutoa taarifa za ukatili wa kijinsia

Image
Na. Dennis Gondwe, CHAMWINO WANAFUNZI wa shule za msingi mkoani Dodoma wametakiwa kutoa taarifa kwa Dawati la Jinsia na Watoto pindi watakapofanyiwa ukatili wa kijinsia ili kuwa na jamii isiyo na ukatili wa kijinsia. Mkaguzi wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma, Theresia Mdendemi akiongea na wanafunzi Kauli hiyo ilitolewa na Mkaguzi wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma, Theresia Mdendemi, kutoka Dawati la Jinsia na Watoto Mkoa wa Dodoma alipokuwa akiongea na wanafunzi wa Shule ya Msingi Chamwino katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Insp. Mdendemi alisema “watoto wazuri msisite kutoa taarifa kwa Dawati la Jinsia na Watoto katika Jeshi la Polisi na watu mnaowaamini pindi mnapofanyiwa ukatili wa kijinsia. Hakikisha ndani ya saa 72 mmetoa taarifa kwenye Dawati la Jinsia na Watoto au mtu mnaemwamini ili tuweze kupata Ushahidi. Mtuhumiwa tunatakiwa tumuunganishe kosa alilofanya na ushahidi tutakaopata toka kwenye mwili wako”. Alisema kuwa mara nyingi ukatili umekuwa ukifanyika kwa watu wa...