Posts

Showing posts from February 7, 2025

Wafanyabiashara wa Soko Kuu la Majengo Dodoma watarajia makubwa Mradi wa TACTIC

Image
Na. Halima Majidi, DODOMA Wafanyabiashara wa Soko Kuu la Majengo Jiji la Dodoma,   wameishukuru serikali kwa kuona umuhimu wa kukarabati miundombinu ya Soko hilo na kuomba   kuharakishwa uboreshaji wa soko ili waweze kuendelea na majukumu yao,   kwa sababu soko hilo ndio soko mama la chakula. Akizungumza katika hafla ya Utiaji Saini Mikataba ya Ujenzi wa Miradi ya TACTIC uliofanyika katika Bustani ya Chinangali Park, Mfanyabiashara wa   Soko Kuu   la Majengo, Rhoda Boyi, alipongeza juhudi za   Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kuwashirikisha   katika hatua zote za mradi "Tunatarajia kuwa sauti zetu zitasikilizwa na kuzingatiwa ili kuhakikisha kuwa maboresho haya yanakidhi mahitaji yetu na kuboresha mazingira ya biashara" alisema Boyi. Kwa upande wake   Mohammedi,   alifafanua changamoto watakazokumbana nazo   katika kipindi chote cha ukarabati wa jengo hilo, ni pamoja na; kupoteza wateja, kuharibika kwa bidhaa kutokana na kuhamishw...

Wakandarasi Wasiomaliza Miradi Mashakani

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA TARURA imeagizwa kuwasimamisha wakandarasi wasiokamilisha miradi kwa wakati na wasipewe tena miradi hiyo kwasababu wanakwamisha juhudi za Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati na ya kimaendeleo nchini. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mohamed Mchengerwa (Mb) Hayo yalisemwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mohamed Mchengerwa (Mb) alipokuwa akizungumza na wataalam kutoka taasisi mbalimbali za kiserikali pamoja na wananchi wa Jiji la Dodoma katika Hafla ya utiaji saini mkataba wa uboreshaji Soko Kuu la Majengo pamoja na ujenzi wa Kituo cha Daladala eneo la Mshikamano, Kizota na Nzuguni, uliofanyika tarehe 06 Februari, 2025 katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma. “Maelekezo yangu kwa TARURA, mkandarasi huyu asiruhusiwe kufanya kazi yoyote chini ya TARURA kuanzia sasa mpaka akamilishe mradi huu tunaoukusudia. Nenden...

Miundombinu ni nyenzo ya maendeleo ya Jiji la Dodoma

Image
Na. Shahanazi Subeti, DODOMA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) pamoja na   Halmashauri ya Jiji la Dodoma zilisaini mkataba wa TACTIC   wenye thamani ya shilingi Bilioni 14.2 kwa lengo la kuboresha miundombinu, kuimarisha usimamizi wa uendelezaji miji na kuboresha mazingira ya uwekezaji ili kukuza uchumi wa halmashauri ya jiji. Hafla hiyo ya Utiaji saini ilifanyika bustani ya Chinangali Park jijini Dodoma katika hafla ya utiaji saini mkataba wa ujenzi wa soko kuu la majengo pamoja na ujenzi wa kituo cha daladala eneo la Mshikamano, Kizota na Nzuguni. Akielezea tukio hilo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mohamed Mchengerwa alisema, mikataba hii itakwenda kuleta mapinduzi makubwa ya kiuchumi kwa watanzania wanaoishi Dodoma na aliwaomba wakandarasi kutekeleza majukumu yao kwa wakati. "Tunapoboresha miundombinu hii itawafanya watanzania na wafanyabiashara, kuweza kusogeza biashara zao karibu, kuweza kutum...

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Image
Na. Aisha Ibrahim, DODOMA Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa (Mb), aliwapongeza watumishi wa umma kwa kusimamia miradi mbalimbali jijini Dodoma ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan. Aliyasema hayo katika Hafla ya utiaji saini mkataba wa ujenzi wa Soko Kuu la Majengo pamoja ujenzi wa kituo cha daladala eneo la Mshikamano, Kizota na Nzuguni, iliyofanyika kiwanja cha Chinangali Park, Jijini Dodoma. Akizungumzia kuhusu utekelezaji wa miradi mbalimbali Mohamed Mchengerwa, alitaka wakandarasi wote ambao hawajatekeleza majukumu yao katika miradi mbalimbali ikiwemo mradi wa ujenzi wa barabara, kutopewa   fursa ya kufanya kazi yoyote   ikiwa ni onyo kwa wale wote wanaofanya kazi kwa uzembe na kushindwa kutekeleza majukumu yao kwa wakati. "Maelekezo yangu kwa mtendaji mkuu na katibu mkuu wa TARURA, Mkandarasi huyu asiruhusiwe kufanya kazi yoyote chini ya TA...

Wananchi washuhudia utiaji saini mkataba wa mradi wa TACTIC

Image
Na. Coletha Charles, DODOMA Wananchi wa Jiji la Dodoma wamejitokeza kwa wingi kushuhudia hafla ya utiaji saini mkataba wa Mradi wa “Tanzania Cities Transforming Infrastructure and Competitiveness” (TACTIC), unaolenga kuboresha na kujenga miundombinu muhimu katika jiji hilo ikiwa ni pamoja na Uboreshaji wa Ujenzi wa Soko, Vituo vya daladala pamoja na vivuko. Hafla hiyo, iliyofanyika katika viwanja vya Chinangali, inahusisha uboreshaji wa Soko Kuu la Majengo, Kituo cha Daladala Mshikamano, Stendi ya mabasi madogo eneo la Kizota, ujenzi wa stendi ya mabasi madogo eneo la Nzuguni, pamoja na ujenzi wa vivuko katika maeneo ya Chadulu, Mailimbili, na Ntyuka. Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Mgeni Rasmi ambaye ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa (Mb), aliwaomba watanzania kuitunza miradi hiyo inayotekelezwa kwenye majiji na miji zaidi ya 45 kwasababu ina thamani kubwa zaidi ya Trilioni 1.1. Alisema kuwa mkataba huo wa bilioni 14.2 wa kuboresha na kujenga m...