Wajasiriamali wanufaika na Nishati Jadidifu Dodoma
Na. Faraja Mbise, DODOMA Wajasiriamali kutoka kata za pembezoni za Hombolo Makulu, Ipala, Mbalawala, Chihanga na Mnadani katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamenufaika na mradi wa nishati jadidifu kwa matumizi ya uzalishaji uliolenga kuimarisha na kuboresha miradi ya wajasiriamali wa pembezoni. Afisa Maendeleo ya Jamii katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Santiel Mmbaga Hayo yalisemwa na Afisa Maendeleo ya Jamii katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Santiel Mmbaga wakati wa mkutano na wadau mbalimbali wenye lengo mahususi la utoaji taarifa ya utekelezaji wa mradi wa matumizi ya nishaji jadidifu kwa matumizi ya uzalishaji kwa mwaka 2022 hadi 2024 katika ukumbi wa Maktaba ya Mkoa wa Dodoma. Mmbaga alisema “halmashauri imeweza kunufaika sana na miradi hii ya Kakute ambayo imetufungia nishati hii jadilifu kwenye maeneo ya pembezoni, kwasababu wananchi wetu walikuwa wanahitaji huduma, walikuwa wanafanya kilimo, walikuwa wanachajisha simu lakini sio kwa kiwango hicho. Lakini saizi k...