Posts

Showing posts from November 14, 2024

Wajasiriamali wanufaika na Nishati Jadidifu Dodoma

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Wajasiriamali kutoka kata za pembezoni za Hombolo Makulu, Ipala, Mbalawala, Chihanga na Mnadani katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamenufaika na mradi wa nishati jadidifu kwa matumizi ya uzalishaji uliolenga kuimarisha na kuboresha miradi ya wajasiriamali wa pembezoni. Afisa Maendeleo ya Jamii katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Santiel Mmbaga Hayo yalisemwa na Afisa Maendeleo ya Jamii katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Santiel Mmbaga wakati wa mkutano na wadau mbalimbali wenye lengo mahususi la utoaji taarifa ya utekelezaji wa mradi wa matumizi ya nishaji jadidifu kwa matumizi ya uzalishaji kwa mwaka 2022 hadi 2024 katika ukumbi wa Maktaba ya Mkoa wa Dodoma. Mmbaga alisema “halmashauri imeweza kunufaika sana na miradi hii ya Kakute ambayo imetufungia nishati hii jadilifu kwenye maeneo ya pembezoni, kwasababu wananchi wetu walikuwa wanahitaji huduma, walikuwa wanafanya kilimo, walikuwa wanachajisha simu lakini sio kwa kiwango hicho. Lakini saizi k...

Wajasiriamali Jiji la Dodoma wahimizwa kurasimisha biashara zao

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Wajasiriamali katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamehimizwa kurasimisha biashara zao kwa lengo la kuwa na wigo mkubwa wa kuweza kukopa katika taasisi za kifedha kwa sababu watakuwa wanatambulika kwa mujibu wa sheria. Katibu Mtendaji wa Shirika Kakute Projects, Livinus Manyanga akiongea na wadau Hayo yalisemwa na Katibu Mtendaji wa Shirika Kakute Projects, Livinus Manyanga alipokuwa akizungumza na wanufaika wa mradi wa nishati jadidifu, wadau wa serikali, viongozi wa sekta ya biashara na wazalishaji wa teknolojia katika mkutano wa wadau wa mradi wa nishati jadidifu kwa matumizi ya uzalishaji uliofanyika katika ukumbi wa Maktaba ya Mkoa uliyopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma. “Tumejaribu kufanya kazi kwa karibu sana na vile vikundi ambavyo vimekopeshwa mikopo na halmashauri tofauti na hii misaada ambayo tumeitoa sisi, inaonesha wazi kwamba changamoto namba moja ni kwamba, mjasiriamali mdogo mpaka aweze kurasimisha biashara yake ni hatua ndefu na hawapendi...