Posts

Showing posts from November 16, 2023

KAMATI YA SIASA MKOA WA DODOMA YAPONGEZA USIMAMIZI UJENZI SHULE YA MIYUJI B

Image
Na. Dennis Gondwe, MIYUJI KAMATI ya Siasa ya Mkoa wa Dodoma imepongeza usimamizi mzuri wa shule mpya inayojengwa ya Miyuji B iliyopo Kata ya Miyuji jijini Dodoma na kusema kuwa shule hiyo itawapunguzia hadha ya kutembea umbali mrefu wanafunzi. Katibu wa CCM Mkoa wa Dodoma, Pili Mbaga akisisitiza jambo Pongezi hizo zilitolewa na Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Dodoma, Pili Mbaga alipoongoza Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Dodoma kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa shule mpya ya Miyuji B inayojengwa Kata ya Miyuji. Mbaga alisema “nimpongeze mkuu wa shule jirani ya Miyuji anayesimamia ujenzi wa shule hii kwa kazi nzuru na usimamizi mzuri. Hakika majengo ni mazuri na yanapendeza. Aidha, niwapongeze na wahandisi kwa kusimamia vizuri shule hii. Maeneo mengine wahandisi hawasimamii miradi ya ujenzi jambo linalopelekea miradi mingi kujengwa chini ya kiwango kwa kukosa usimamizi”. Vilevile, kiongozi huyo wa Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Dodoma alielezea kufurahishwa kwake kwa taa...

NYUMBA YA WALIMU YAJENGWA KWA VIWANGO SHULE YA MTEMI CHILOLOMA

Image
  Na. Dennis Gondwe, DODOMA KAMATI ya Siasa ya Mkoa wa Dodoma imeridhishwa na viwango vya ujenzi wa nyumba ya walimu ‘two in one’ katika Shule ya Sekondari Mtemi Chiloloma na kusema kuwa utakuwa imejengwa kwa viwango bora. Katibu wa CCM Mkoa wa Dodoma, Pili Mbaga akiongea na umma baada ya kukagua ujenzi wa nyumba ya walimu (two in one)  Kauli hiyo ilitolewa na Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Dodoma, Pili Mbaga alipoongoza Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Dodoma kutembelea na kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Mbaga alisema kuwa Kamati ya Siasa Mkoa wa Dodoma imeridhishwa na ujenzi wa nyumba ya walimu shuleni hapo. “Mradi wa ujenzi wa nyumba ya walimu ni nzuri na umejengwa na kusimamiwa vizuri. Huko zamani wahandisi walikuwa nyuma katika kusimamia miradi ya ujenzi, lakini siku hizi wapo mstari wa mbele na wanafika katika kusimamia miradi ya ujenzi. Jukumu letu ni kuwaambia wananchi kazi nzuri inayofanywa...

UJENZI WA NYUMBA YA WALIMU SHULE YA MTEMI CHILOLOMA MSAADA KWA WALIMU

  Na. Dennis Gondwe, DODOMA MRADI wa ujenzi wa nyumba ya walimu (mbili kwa moja) katika shule ya Sekondari Mtemi Chiloloma utawasaidia walimu kukaa mazingira ya shule jambo litakaloongeza ufanisi katika utendaji kazi wao na kutoa matokeo chanya. Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Shule ya Sekondari Mtemi Chiloloma, Mwl. Livinus Tanganyika alipokuwa akisoma taarifa ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa nyumba ya walimu (two in one) katika Shule ya Sekondari Mtemi Chiloloma iliyopo Kata ya Hombolo Makulu Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Mwl. Tanganyika alisema kuwa serikali kupitia mradi wa kuboresha shule za sekondari (SEQUIP) ilitoa jumla ya shilingi 95,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya walimu ambapo lilikuwa ni hitaji kubwa kwa sababu eneo la shule liko mbali na eneo la makazi ya watu. Fedha za ujenzi ziliingizwa katika akaunti ya shule tarehe 20/6/2023 na kuvuka mwaka na kuanza kutumika katika mwaka wa fedha 2023/2024. Akiongelea utekelezaji wa mradi huo alisema kuwa uli...