Posts

Showing posts from March 13, 2025

Dodoma Jiji FC, yatua Dar kibabe kumenyana na Mnyama

Image
Na. Mussa Richard, Klabu ya Soka ya Dodoma Jiji FC, itashuka dimbani hapo kesho kumenyana na klabu ya Soka ya Simba SC, katika mchezo wa ligi kuu ya NBC Tanzania bara, mchezo utakaopigwa katika dimba la KMC Complex Mwenge, Dar es salaam majira ya saa 10 kamili jioni. Akizungumzia maandalizi ya timu, Kocha mkuu wa Dodoma Jiji FC, Mecky Mexime wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuelekea mchezo wa Simba SC, alisema ā€œtunamshukuru Mungu tumefika Dar es Salaam salama, jana tumefanya mazoezi mepesi ya kuiweka miili sawa, tunajua mchezo utakuwa ni mgumu kwa pande zote, ukizingatia kwasasa ligi inaelekea ukingoni. Alama tatu kwa kila mchezo ni muhimu ili tuweze kifikia malengo yetu ya kumaliza ligi tukiwa nafasi za juu kwenye msimamo, maandalizi yote ya kucheza na Simba SC, tumeyafanya tukiwa Dodoma. Hapa tumekuja kukifanyia kazi kile tulichojifunza kwenye uwanja wa mazoeziā€™ā€™. Nae Abdi Banda, mchezaji wa Klabu ya Soka ya Dodoma Jiji FC, akawaita mashabiki wa Dodoma Jiji FC, waliopo Da...

Habari Picha, Lishe wanafunzi wa Awali Shule ya Msingi Mlezi

Image
  Wanafunzi wa Awali katika Shule ya Msingi Mlezi wakipata uji shuleni hapo wakati wa asubuhi

Habari Picha ya Lishe Shule ya Msingi Mlezi

Image
  Watoto wenye mahitaji maalum wa Shule ya Msingi Mlezi wakipata chakula cha mchana mara baada ya masomo yao

Wazazi watakiwa kutoa kipaumbele kwa maendeleo ya watoto

Image
Na. Leah Mabalwe, HAZINA   Diwani wa Kata ya Hazina, Samwel Mziba, amewataka wazazi pamoja na walezi kuwa kipaumbele katika maendeleo ya watoto wao shuleni.   Mziba, alisema hayo wakati wa kikao cha walimu pamoja na wazazi kilichofanyika katika Shule ya Msingi Mlezi kwa lengo la kuzungumzia maendeleo ya lishe bora kwa wanafunzi wa shule hiyo. ā€œKwanza kabisa napenda kuwashukuru wazazi wote mliofika katika kikao hiki, najua mnaelewa lengo na dhumuni la kuitisha kikao hiki cha leo, tukianzia kuzungumzia suala zima la malezi kwa watoto, tunashuhudia wazazi wengi wanakuwa wametingwa sana na kazi zao, kiasi kwamba wanakua hawana muda wa kufuatilia maendeleo ya watoto wao shuleni. Hii hali si nzuri kwasabu inamjengea mtoto kufanya kila kitu anachojisikia kwa vile hakuna mtu yeyote anae weza kummfuatilia. Hivyo, basi napenda kuwahamasisha wazazi pamoja na walezi tuwe mstari wa mbele kufuatilia maendeleo ya watoto wetu shuleniā€™ā€™alisema Mziba. Pia aliongezea kwa kuwataka wazaz...

Mavunde apongeza Baraza la madiwani kupendekeza kugawanywa Jimbo la Dodoma Mjini

Image
  Na. Nancy Kivuyo Mbunge wa Jimbo la Dodoma mjini, Anthony Mavunde, ametoa pongezi kwa baraza la madiwani kwa kuridhia taarifa ya mapendekezo ya mgawanyo wa Jimbo la Uchaguzi la Dodoma Mjini kuwa majimbo mawili. Katika salamu zake fupi aliishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa mabadiliko makubwa katika sekta mbalimbali. Akizungumzia mgawanyo wa Jimbo la uchaguzi la Dodoma Mjini na kuwaeleza madiwani faida zitakazopatikana baada ya kugawanya kwa jimbo hilo. ā€œJimbo la Dodoma mjini ndilo jimbo kubwa kuliko majimbo yote hapa nchini likiwa na Tarafa nne, kata 41 na mitaa 222. Nipende kuwaambia, mgawanyo wa jimbo utaongeza fursa nyingi za kuhudumia wananchi. Mfuko wa jimbo utasogeza huduma kwa jamii kwa urahisi zaidi, kupitia uwepo wa majimbo mawili, fedha nzuri itapatikana kwa ajili ya kuboresha miundombinuā€ alisema Mavunde. Aliongeza kuwa mipango ya kiserikali inasaidia huduma za kijimbo kupatika...

Wapiga kura 795,000 Kugawanywa, Jimbo la Dodoma Mjini

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma yawasilisha mapendekezo ya kugawanya Jimbo la Uchaguzi la Dodoma Mjini lenye jumla ya wapiga kura 795,000 na kuwa majimbo mawili, Jimbo la Mtumba lenye jumla ya wapiga kura 412,000 na Jimbo la Dodoma Mjini lenye jumla ya wapiga kura 383,000 kwa lengo la kusogeza huduma karibu na wananchi. Hayo yalisemwa na Afisa Uchaguzi wa Halmashauri hiyo, Albert Kasoga alipokuwa akiwasilisha taarifa kwa niaba ya Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, ya mapendekezo ya mgawanyo wa Jimbo la Dodoma Mjini, mbele ya Mkutano maalum wa Baraza la Madiwani uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Akizungumza wakati wa kuwasilisha taarifa hiyo, alisema kuwa mgawanyo huo umezingatia hali ya kiuchumi ya jimbo husika hasa katika ukusanyaji wa mapato ya ndani sambamba na kuzingatia ukubwa wa eneo husika. ā€œMgawanyo umezingatia hali ya kiuchumi ya jimbo hasa katika ukusanyaji wa mapato ya ndani ya jimbo husika. Lengo ni kuona kuwa maene...