Posts

Showing posts from July 5, 2024

Kituo cha Afya Ilazo mkombozi kwa wananchi

  Na. Mwandishi wetu MRADI wa ujenzi wa Kituo cha Afya Ilazo utakapokamilika utahudumia wananchi 99,743 wa Kata ya Nzuguni na maeneo ya jirani ikiwa ni mkakati wa serikali ya awamu ya sita wa kusogeza huduma za afya karibu na wananchi. Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Andrew Method alipokuwa akisoma taarifa mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya Ilazo kwa Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2024. Dkt. Method alisema kuwa lengo la mradi huo ni kuboresha huduma za mama na mtoto na huduma za upasuaji ukitarajiwa kuhudumia zaidi ya wananchi 99,743 wa Kata ya Nzuguni, Ipagala na maeneo menginge watapata huduma bora za afya mradi huo utakapokamilika. Akiongelea mafanikio ya mradi huo, aliyataja kuwa ni kuwezesha kutoa huduma za upasuaji, kliniki ya mama na mtoto, huduma za kujifungua, wodi ya watoto wachanga , huduma za kuhifadhi miili. Mafanikio mengine ni “wodi hizi pia zimeunganishwa na mi...

Dodoma English Medium kusomesha kwa gharama nafuu

  Na. Mwandishi wetu, MRADI wa ujenzi wa Shule ya Awali na Msingi Dodoma English Medium umewasaidia wazazi wenye kipato cha kati kusomesha watoto wao katika shule ya mchepuo wa kiingereza karibu na maeneo yao kwa gharama nafuu. Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prisca Myalla alipokuwa akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa Shule ya Awali na Msingi ya Dodoma English Medium kwa Kiogozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2024. Akiongelea faida za mradi huo alizitaja kuwa ni kuwasaidia wazazi wenye kipato cha kati kupata fursa ya kusomesha watoto kwenye shule ya mchepuo wa ki i ngereza . Faida nyingine aliitaja kuwa ni wananchi kusogezewa huduma ya shule karibu ambapo watoto walikuwa wanasafiri umbali mrefu kufuata huduma ya elimu pia wanafunzi wanapata elimu bora kwa gharama nafuu ukilinganisha na shule binafsi . “ Ndugu Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2024, m radi umelenga kutoa elimu bora amb...

BAgamoyo Garden kuipendezesha Dodoma

  Na. Mwandishi wetu, MRADI wa Bagamoyo Garden wa utunzaji na uhifadhi wa mazingira kwa njia ya upandaji miti, maua na nyasi unalenga kuunga mkono juhudi za serikali za kuifanya Dodoma kuwa ya kijani na inayopendeza. Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa mradi wa Bagamoyo Garden, Rogasian Malya alipokuwa akisoma taarifa ya mradi wa Bagamoyo Garden wa utunzaji na uhifadhi wa mazingira kwa njia ya upandaji miti, maua na nyasi katika eneo la wazi kwa Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2024. Malya alisema kuwa lengo la mradi huo ni kuunga mkono juhudi za s erikali za kuifanya Dodoma kuwa ya kijani kwa njia ya upandaji miti , k ampeni ambayo ilizinduliwa mwaka 2021 kwa kupanda miti katika chanzo cha maji Mzakwe na aliyekuwa Makamu wa Rais ambaye kwa sasa ndiye Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Mhe shimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan. Alisema kuwa m radi hu o unatekeleza kwa vitendo ujumbe wa m bio za Mwenge wa Uhuru, 2024 usemao ‘ Tunza Mazingira na Shirik...

Mwenge wa Uhuru waweka jiwe la msingi Dodoma Media Group

  Na. Mwandishi Wetu Kituo cha vyombo vya habari cha Dodoma Media Group kutoa elimu ya mpiga kura katika kujiandaa na uchaguzi wa serikali za mitaa na utunzaji wa mazingira. Kauli hiyo ilitolewa na Mejena Mkuu wa Dodoma Media Group, Zania Miraji alipokuwa akisoma taarifa ya mradi wa kituo cha vyombo vya habari cha Dodoma Media Group kilichopo katika Mtaa wa Miyuji Proper jijini Dodoma kwa Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2024. Miraji alisema “ kupitia vyombo vya habari vya Dodoma Media Group jamii ya Dodoma itapata haki ya upatikanaji wa taarifa na elimu juu ya masuala mbalimbali ikizingatia ujumbe wa ‘ Tunza Mazingira na Shiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Ujenzi wa Taifa E ndelevu ’ . Elimu itakayotolewa ni pamoja na elimu ya masuala ya uchaguzi ikiwemo elimu ya mpiga kura ambapo kutakuwa na kipindi maalum cha kuelimisha Umma kujiandaa na uchaguzi wa s erikali za m itaa. Pia itatolewa elimu juu ya lishe na kutakuwa na kipindi maalum kitakachozungumzia...

Barabara ya Judiciary kupunguza msongamano katikati ya Jiji la Dodoma

Image
Na. Dennis Gondwe, TAMBUKARELI UJENZI wa barabara ya ‘Judiciary’ yenye urefu wa kilometa mbili unalenga kupunguza msongamano wa magari katikati ya Jiji la Dodoma na kuharakisha huduma kwa wananchi. Kauli hiyo ilitolewa na Meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Wilaya ya Dodoma, Mhandisi Emmanuel Mfinanga wakati akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa barabara ya Judiciary yenye urefu wa kilometa mbili kwa kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa. Mhandisi Mfinanga alisema ”n dugu kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa 2024, lengo la mradi huu ni kupunguza msongamano wa magari katikati ya Jiji la Dodoma, kurahisisha huduma kwa wananchi katika ofisi zilizopo katika eneo hili ambapo miongoni mwa ofisi hizo ni:- Ofisi ya Bima (NHIF), Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Wakala wa Ununuzi Tanzania (PPRA), Ofisi za Maadili ya Viongozi wa Umma na Ofisi za Mahakama Kuu ya Tanzania”.   Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa, Godfrey Mnzav...