Posts

Showing posts from December 18, 2024

Madiwani wadaiwa uthubutu kufanya maamuzi ya kimaendeleo

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa, mkoani Kagera, wametakiwa kuwa na uthubutu katika kufanya maamuzi ya kimaendeleo ili kuwanufaisha wananchi wanaowasimamia. Hayo yalisemwa na Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe, alipokuwa akiwakaribisha madiwani kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa, mkoani Kagera, katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Mstahiki Meya, Prof. Davis Mwamfupe akifafanua jambo “Kikubwa katika mtakachokiona, sio utajiri wetu wa pesa ni uthubutu wa kufanya maamuzi, unaweza kuwa na pesa lakini hauna uthubutu wa kuzitumia, ukipewa shilingi milioni moja, utapata wasiwasi kuzitumia kwasababu zitaisha, hutakubali matumizi ya laki mbili au tatu. Lakini sisi hatuogopi, kama tuna mradi wa hoteli iliyopo hapa ambayo imegharimu shilingi Bilioni 12, hatuogopi mradi wa Soko la wazi la Machinga, ingawa serikali ilituchangia shilingi Bilioni tatu, na sisi tukaweka shilingi bilioni sita nyingine. Hatuogopi kwamb...

Wataalam watumike kukuza mapato ya ndani

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Mamlaka za Serikali za Mitaa zimetakiwa kuwajengea uwezo wa kimbinu na kuwatumia wataalam wa ndani ili kuongeza mapato ya ndani sambamba na kubuni miradi ya kimkakati yenye tija kwa maendeleo ya nchi. Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko akifafanua jambo kwa mfano Hayo yalisemwa na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipokuwa akizungumza na Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa, waliotembelea Dodoma kwa lengo la kujifunza na kuongeza wigo wa namna sahihi ya kuongeza mapato ya ndani kupitia miradi mbalimbali, katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. “Hakuna mapato madogo na hakuna mradi mdogo, ila tunapoandaa miradi, tujiulize tunaandaa miradi yenye mfumo gani?. Kwahiyo, tunavyofikiri miradi, hata yenye mtazamo wa kibiashara lazima tufikirie kwenye kukua kwake. Hivyo, kila kitu kinaweza kikaanza kwenye udogo, kikakua na mapato yaleyale madogo tunaweza tukaanzisha miradi kwa mapato ya ndani. Nilicho...