Posts

Showing posts from October 8, 2024

Mradi wa majaribio wa usimamizi taka kuanza Dodoma

Image
Na. Asteria Frank, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kushirikiana na Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira wanatekeleza mradi wa majaribio wa usimamizi wa taka za plastiki katika Jiji la Dodoma kwa lengo la kuhamasisha njia bunifu katika usimamizi wa taka za plastiki kupitia dhana ya uchumi rejeshi ili kupunguza taka za plastiki kwenye mazingira na kuboresha maisha na uchumi wa taifakwa ujumla. Baada ya kutembelea na kukagua maendeleo ya mradi huo uliopo katika Kata ya Chamwino, Afisa Mazingira wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Aliy Mfinanga, alisema kuwa mradi wa majaribio utawanufaisha na kuwawezesha jamii na vikundi vya usafi kufanya shughuli za ukusanyaji na usafirishaji wa taka katika Kata ya Chamwino kwa nia ya kutia thamani kupitia dhana ya uchumi rejeshi ili kutunza Mazingira kutokana na plastiki. “Tumeshazoea kuona msisitizo mkubwa kuwa taka ni taka na kwamba haifai tena, lakini kupitia mradi huu wa majaribio tunataka kuonesha jamii kuwa tunaweza kuongeza...

Maafisa Waandikishaji waaswa uadilifu

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Maafisa waandikishaji orodha ya wapiga kura uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2024 Halmashauri ya Jiji la Dodoma wameaswa kuwa waadilifu ili Dodoma iwe ya kwanza kwa idadi kubwa ya watu walioandikishwa. Mjumbe wa Kamati ya Uratibu wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma, Coletha Kiwale Hayo yalisemwa na Mjumbe wa Kamati ya Uratibu wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma, Coletha Kiwale wakati akizungumza na maafisa waandikishaji, watendaji wa mitaa, wasimamizi wasaidizi ngazi ya kata pamoja na maafisa watendaji wa kata wakati wa mafunzo kwa maafisa waandikishaji wa orodha ya wapiga kura leo katika ukumbi wa Mtumba Complex jijini Dodoma. Kiwale aliwataka maafisa waandikishaji kuwa weledi na wenye ufanisi katika suala la muda, mavazi na utoaji taarifa kwa wakati. Msisitizo mwingine alisisitiza wawe waadilifu na wahamasishaji kwa waandikishaji kujitokeza kwa wingi katika kujiandikisha kwenye orodha ya wapiga kura. “Napenda tushirikishane ...