Posts

Showing posts from January 25, 2025

Timu ya Pete ya Combine yatubu kwa Timu ya Elimu Msingi

Na. Coletha Charles, DODOMA Timu ya Mpira wa Pete ya Elimu Msingi imeibuka na ushindi wa kishindo kwa kuifunga Timu ya Combine (Elimu Sekondari na Watendaji wa kata) kwa mabao 9-5 ambapo mchezo huo ulifanyika kwenye uwanja wa Jamhuri, ukiwa na ushindani mkubwa huku kila upande ukionesha mchezo wa hali ya juu. Mchezo ulianza kwa kasi huku Timu ya Elimu Msingi ikiongoza katika robo ya kwanza kwa mabao 4-1 wakitumia uzoefu wa wachezaji wao wakongwe. Hata hivyo, Combine walionesha nidhamu ya hali ya juu na kutumia mbinu bora za kiufundi, katika robo ya pili timu zote ziliongeza kasi ili kupata alama muhimu za ushindi huo wa kihistoria. Kocha wa timu ya Elimu Msingi, Emma Ernest, alisema kuwa, walishinda kwa sababu nyumba bila msingi hauwezi kujenga. Hivyo, waliweka msingi imara ndio maana waliweza kushinda kwa kishindo kwa kufanya mazoezi. “ Tulijiandaa vya kutosha kwa mchezo huu. Wachezaji wangu wameonyesha nidhamu, umoja, na uwezo wa kupambana hadi dakika ya mwisho. Ushindi huu ni ...

Maandalizi ya Jarida la Bonanza la Jiji la Dodoma

Image
  Mtaalam wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Jiji la Dodoma Aisha Haji akifanya mahojiano na Mchezaji wa Timu ya Kuvuta Kamba Wanawake ya Jiji la Dodoma, Devotha Selufara katika Uwanja wa Jamhuri

Kamba wanaume Ofisi ya Rais Ikulu yaiburuza kwa taabu Ofisi ya Rais Jiji la Dodoma

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Timu ya Kuvuta Kamba wanaume kutoka Ofisi ya Rais Ikulu imeiburuza kwa taabu sana Timu ya Kuvuta Kamba wanaume ya Ofisi ya Rais Jiji la Dodoma kwa mivuto miwili mtawalia katika Bonanza la michezo. Katika mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini hapa, timu zote zilionesha kukamiana kutokana na kuwa chini ya mwavuli mmoja ambao ni Ofisi ya Rais. Aidha, mwamuzi wa mchezo huo alilazimika mara kadhaa kutumia filimbi yake kuzikumbusha timu zote mbili kanuni za mchezo huo wa kiuvuta kamba. Mchazo ulianza kwa nguvu na kila upande ulionesha unaweza ibuka mshindi. Ofisi ya Rais Ikulu iliibuka kidedea kwa kuiburuza kwa taabu sana Ofisi ya Rais Jiji la Dodoma kwa mivuto miwili bila majibu. Halmashauri ya Jiji la Dodoma iliandaa Bonanza la michezo mbalimbali la wafanyakazi kwa lengo la kuwakutanisha na kufurahia kuuaga mwaka 2024 na kuukaribisha mwaka 2025 katika Uwanja wa Jamhuri Dodoma. MWISHO

Mkurugenzi wa Jiji awatakia Heri ya Mwaka Mpya 2025 Wafanyakazi

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA MKURUGENZI wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko amewatakia heri ya mwaka mpya 2025 wafanyakazi wote katika Bonanza kubwa michezo katika uwanja wa Jamhuri Dodoma. Akifungua bonanza hilo lililoandaliwa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa ajili ya kuwakutanisha wafanyakazi na kuuaga mwaka 2024 na kuukaribisha mwaka 2025, Mkurugenzi wa Jiji alisema kuwa michezo inalenga kuwakutanisha wafanyakazi na kuwakumbusha kuwa ni wamoja na wanatakiwa kufanya kazi kwa upendo na kushirikiana. Akiongelea umuhimu wa michezo katika kujenga urafiki na umoja alisema kuwa hilo halina mjadala. “Karibu sana katika uwanja wa Jamhuri. Tumekutana hapa taasisi zaidi ya moja katika uwanja huu lakini wote lengo letu ni moja la michezo kwa afya zetu. Ushauri wangu Dodoma Jiji wenye ratiba wakutane na Ofisi ya Rais, Ikulu ‘kuharmonise’ ratiba ili tuona tutakavyoshirikiano pamoja. Heri ya Mwaka mpya 2025” alisema Dkt. Sagamiko. Kwa upande wake Mwl. Sylvia Madeje kut...