Posts

Showing posts from December 16, 2024

Wananchi watakiwa kuwa msitari wa mbele kupinga ukatili

Na. Coletha Charles, CHAMWINO Wakazi wa Kata ya Chamwino, Halmashauri ya Jiji la Dodoma walipewa elimu dhidi ya ukatili wa kijinsia na malezi bora ambayo imetolewa katika Ofisi ya Afisa Mtaa wa Mwaja kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kutambua yanayoendelea kwenye jamii.   Akizungumza na wakazi wa eneo hilo, Mratibu wa Jinsia na Watoto, Fatuma Kitojo amewataka wazazi hao kuwa walezi bora kwa watoto wao na kutowatamkia maneno mabaya ambayo yanawakatili kisaikolojia ili wakubalike na jamii inayo wazunguka. Kitojo alisema kuwa ni muhimu kwa wazazi kuelewa kwamba maneno wanayosema yanaweza kuwa na athari kubwa kwa maendeleo ya watoto kihisia, kujitambua, na uhusiano mzuri na Watoto wengine. “Watoto wetu wanatupenda sana na wanapenda kuona sisi tunafanikiwa ni kweli tuna shughuli nyingi tunakimbizana na muda na maisha kwa sababu za hali za kiuchumi na mabadiliko ya sayansi na teknolojia. lakini tunajua kwa asili mwanamke ndiyo mlezi namba moja. Kwahiyo tunatakiwa tutenge mda wa ...

RC Senyamule azipongeza Club za Jogging Dodoma

Image
Na. John Masanja   Vikundi vya 'Jogging C lub s ' Mkoa wa Dodoma vimepongezwa kwa kuendelea kuwa na mshikamano na kuwa vinara wa kuhamasisha watu kufanya mazoezi kwa kuboresha afya zao na kuepukana na magonjwa yasiyoambukiza, pamoja na kuelimisha jamii kupitia kampeni mbalimbali.    Pongezi hizo zilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule baada ya kumalizika kwa mazoezi na mbio fupi zilizofanyika kwa kuratibiwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma k wa kushirikiana na “ Friends of Mavunde ” na “ Dodoma City L egends Family” .    “ Katika makundi tuliyonayo kwa mkoa wetu hivi vilabu vya Jogging wamekuwa kinara wa kuimarisha m shikamano wao wenyewe na wafuasi sisi tunaoungana nao kufanya mazoezi, ni makundi ambayo hayana uvivu wa kufuatilia jambo lao wakiamua nawapongeza sana.    " Kupitia mchango wao wa kuhamasisha unatupa sisi fursa ya kufikisha ujumbee mbalimbali . Kwa jamii, jambo kubwa nimefurahi leo k wa sababu mazoezi haya...

Bonanza la Mashirika yasiyo ya Kiserikali jijini Dodoma 2024 lafana

Image
Na. John Masanja, DODOMA   Mwakilishi wa Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Neema Kilongola ambaye ni Afisa Michezo wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma ameshiriki katika Bonanza la kufunga m waka la m ashirika yasiyo ya kiserikali (NaCoNGO) Mkoa wa Dodoma.   Aidha , bonanza hilo lenye kaulimbiu isemayo "Mazoezi ni Tiba" limefanyika katika uwanja wa michezo wa Shule ya Sekondari Jamhuri na kuhudhuriwa na wanamichezo na wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya Jiji la Dodoma. Akizungumza na wanamichezo hao, Kilongola alisema kuwa matokeo yanayotegemewa kutokana na bonanza hil o ni ongezeko la aina ya michezo na ushiriki wa jamii katika michezo, ongezeko la uelewa wa jamii na mabadiliko ya tabia juu ya ufanyaji wa mazoezi pamoja na ushuhuda wa watu juu ya kupungua kwa maumivu ya mwili na uzito. Alitoa rai kwa mashirikia yasiyo ya k iserikali kuanzisha uchangiaji wa jamii na wadau ili kuwapa motisha walimu na wataalamu wa afya na manunuzi ya vifaa vya michezo. "Niwasha...