Posts

Showing posts from January 11, 2024

Shule ya Msingi Chinangali wapewa elimu ya Uzalendo

Image
Na. Leah Mabalwe, CHAMWINO Wanafunzi wa shule ya Msingi Chinangali Kata ya Chamwino wapewa elimu juu ya uzalendo wa nchi yao. Hayo yalijili baada ya Afisa Ushilikishwaji wa Jeshi la Polisi Kata ya Chamwino, A/Insp Isiaka Shabani kutembelea shule hiyo na kutoa mafunzo ya uzalendo na kusema kuwa kila wanafunzi ni jukumu lake kuwa mzalendo. “Kila mwanafunzi ni jukumu lake kuwa mzalendo na kuachana na matendo mabaya ambayo yanajikita katika ukatili na badala yake kuwa mzalendo katika Taifa lake kwa kumtolea mfano Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan” alisema A/Insp. Shabani. Aidha, aliongeza kwa kuwataka wanafunzi hao kujua umuhimu wa Bendera ya Taifa maana yake hususani rangi zinazopatikana katika Bendera ya Taifa ni kielelezo kikubwa cha Taifa. Pia alimalizia kwa kuwasihi wanafunzi   hao wa Shule ya Msingi Chinangali kuwa   inapaswa kuwa mzalendo   popote pale watakapo kuwepo na uzalendo huanzia ndani ya moyo wa mtu na kila Mtanzania n...

Mradi wa Polisi Jamii "FAMILIA YANGU HAINA UHALIFU" wapokelewa vizuri Kata ya Chamwino

Image
  SP Dr. Ezekiel Kyogo, kutoka Makao Makuu ya Polisi, Kamisheni ya Polisi Jamii kwa kushirikiana na Afisa ushirikishwaji wa Jeshi la Polisi wa Kata ya Chamwino A/Insp. Isihaka Shabani wameshirikiana kutoa Elimu ya Mradi wa Polisi Jamii unaoitwa "Familia yangu haina Uhalifu" kwa wananchi wa Mtaa wa Mwaja (eneo la Kidongo chekundu), Kata ya Chamwino. Wananchi wamefundishwa kuelimishwa kuepukana na uhalifu ngazi ya familia kama ifuatavyo:-   1. Wananchi wamefundishwa ni changamoto zipi katika ngazi ya familia ambazo hupelekea Mtu kuingia kwenye uharifu lakini pia waliwakumbusha wazazi wawe mfano kwa kuonyesha tabia nzuri ili watoto waige mazuri yao. 2. Ni Muhimu sana wazazi wawe marafiki wa watoto ili kujua changamoto zao pamoja na kuwa na kauli nzuri kwa watoto ili wasikate tamaa na kuingia kwenye makundi ya uhalifu. 3. Wazazi wamehimizwa kuwajenga watoto mapema namna ya kujitegemea ili wawe na tabia ya kupenda kufanya kazi. 4. Wazazi wamekumbushwa kuwa na tabia ya ...