JIJI LA DODOMA LATAMBUA JITIHADA ZA MWANAMKE WA KIJIJINI
Na. Dennis Gondwe, CHIHANGA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma inatambua jitihada zinazofanywa na mwanamke wa kijijini katika uzalishaji wa chakula na kusimamia lishe ya familia. Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii, Charity Sichona Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Charity Sichona alipokuwa akiongea maadhimisho ya siku ya mwanamke anayeishi kijijini ofisini kwake leo ambayo yatafanyika katika Kata ya Chihanga jijini Dodoma. Sichona alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma inaadhimisha siku hiyo kwa lengo la kuendelea kutambua jitihada za mwanamke anayeishi kijijini. āWanawake wanaoishi vijijini wanamchango mkubwa katika kuzalisha chakula na kuchangia uwepo wa chakula katika familia na nchi nzima. Hivyo, serikali imeamua kutambua jitihada zao za kilimo, ufugaji na shughuli za kiuchumi na kuwatia moyo ili waendelee kuzalisha wakati serikali ikiendelea kutatua changamoto zinawakabiliā alisema Sichona. Sichona alisema ku...