Posts

Showing posts from October 23, 2023

WIZARA YA ARDHI KUBORESHA MFUMO WA ILMIS

Image
  Na. Dennis Gondwe, DODOMA WIZARA ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi inaendelea kuboresha mfumo wa kieletroniki wa kutunza taarifa za Ardhi (ILMIS) ili kuboresha utoaji wa huduma ikiwemo kurahisisha upatikanaji wa hati milki ikiwa niutekelezaji maelekezo ya serikali. Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Slaa akiongea na waandishi wa habari Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Slaa alipokuwa akiongea na waandishi wa habari leo katika Ofisi ya Ardhi Mkoa wa Dodoma kuhusu utekelezaji wa maelekezo ya serikali kuhusu kuboresha huduma za sekta ya Ardhi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma na Mwanza. Slaa alisema “tarehe 3 Oktoba, 2023 serikali ilitoa maelekezo mbalimbali yaliyolenga kuboresha huduma za sekta ya Ardhi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma na Mwanza. Maelekezo hayo yalihusu mamlaka mbalimbali zinazohusika na usimamizi wa sekta ya Ardhi. Wizara inaendelea na uboreshaji wa mfumo wa kieletroniki wa kutunza t...

JIJI LA DODOMA LAPEWA HADHI YA MKOA WA ARDHI

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA WIZARA ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi yaipa Halmashauri ya Jiji la Dodoma hadhi ya kuwa Mkoa wa Ardhi kwa lengo la kuboresha huduma kwa wananchi. Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Slaa Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Slaa alipokuwa akiongea na waandishi wa habari leo katika Ofisi ya Ardhi Mkoa wa Dodoma kuhusu utekelezaji wa maelekezo ya serikali kuhusu kuboresha huduma za sekta ya Ardhi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma na Mwanza. Slaa alisema “Wizara imeifanya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuwa Mkoa wa Ardhi kiutendaji ikiwa na Kamishna wa Ardhi Msaidizi ambae atahudumia eneo hilo na halmashauri nyingine kuwa na Kamishna wa Ardhi Msaidizi mwingine”. Waziri huyo alisema kuwa wizara imeandaa utaratibu wa kutoa huduma kwa pamoja katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma utaratibu ambao utasimamiwa na wizara kwa kushirikiana na Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuanzia tarehe 30 Oktoba,...