Kata ya Ipala yatekeleza agizo la usafi wa Mazingira
Na. Mwandishi wetu, IPALA
Zoezi la uhamasishaji wa Usafi wa Mazingira katika
Kanda Namba Saba limekua lenye mafanikio makubwa. Zoezi hilo limefanyika katika
mitaa mitano iliyopo ndani ya Kata ya Ipala Mtaa wa Sokoine, Madukani, Azimio,
Ukombozi na Mwinyi.
Usafi wa Mazingira ulishilikisha wataalamu kutoka Kanda Namba Saba, wenyeviti wa mitaa, Diwani pamoja na wananchi waliojitoa kusafisha mitaa yote mitano kwa ushirikiano mkubwa kufuatia agiza la Mkuu wa Mkoa wa Dodoma la kusafisha Jiji la Dodoma kila siku.
Akizungumza baada ya zoezi la Usafi wa Mazingira, DIwani
wa Kata ya Ipala, Andrew Muhulo aliwapongeza wananchi kwa kujitokeza kwa wingi
katika zoezi hilo la usafi wa Mazingira na kuwasihi wasiishie hapo tu maana
zoezi la usafi ni maisha ya kila siku ya mtu mmoja mmoja.
“Niwapongeze wananchi wote kwa kujitokeza kwenu kwa
wingi mkuu wetu wa mkoa amesema zoezi la usafi ni la kila siku hivyo tudumishe
usafi katika maeneo yote na viongozi kutoka kanda watapita Kwenye maeneo yenu
na kukagua namna usafi unavyofanyika” alisema Muhulo.
Kwa upande wao wataalamu kutoka Kanda Namba Saba wameahidi kuendelea kutoa elimu kwa wananchi katika kata zote na mitaa yote na kuhakikisha wananchi wanakua na uelewa juu ya maswala ya uhifadhi na utunzaji wa Mazingira.
Usafi wa Mazingira katika maeneno yanayotuzunguka, majumbani, maeneo ya taasisi
na sehemu zenye mkusanyiko wa biashara ni muhimu kufanyiwa usafi kwa
kushirikiana wananchi wote, viongozi na wadau wa mbalimbali katika kuhifadhi
Mazingira.
Comments
Post a Comment