Mwezi wa Maendeleo ya Jamii kufungua fursa za kiuchumi kwa Vijana Dodoma


Na. Mwandishi wetu, DODOMA

 

Halmashauri ya Jiji la Dodoma imesema itaendelea kufungua na kuwawezesha vijana kutumia fursa mbalimbali za kiuchumi na kijamii kupitia Mwezi wa Maendeleo ya Jamii, kwa lengo la kuwajengea uwezo na kuwawezesha kujitegemea.


 

Akizungumza kuhusu shughuli zitakazotekelezwa katika Mwezi wa Maendeleo ya Jamii, Afisa Vijana wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Ndulani alisema kuwa moja ya maeneo yatakayopewa kipaumbele ni kuwawezesha vijana kupata fursa za kiuchumi.

 

Aliongeza kuwa fursa hizo ni pamoja na mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa wafanyabiashara wadogo, maarufu kama machinga.

 

“Halmashauri pia itaendelea kutoa elimu ya ujasiriamali na stadi mbalimbali kwa vijana ili kuwajengea uwezo wa kutumia fursa zinazopatikana na kuendeleza shughuli zao za kiuchumi,” alisema Ndulani.

 

Aliongeza kuwa Halmashauri itaendelea kutekeleza Sera ya Maendeleo ya Vijana pamoja na kuwaunganisha vijana na tenda za serikali, hatua inayolenga kuwapa nafasi ya kushiriki katika shughuli mbalimbali za kiuchumi.

 

Vijana wametakiwa kutambua na kutumia fursa zinazopatikana kwa manufaa yao, huku wakihimizwa kushirikiana na kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo ya jamii ili kuchangia maendeleo ya Jiji la Dodoma.

Comments

Popular Posts

Kata ya Miyuji Yaongeza Kasi ya Usimamizi Wa Usafi wa Mazingira

Kata za Nkuhungu na Kizota zajiandaa kukabiliana na mvua za El Nino

Mwenyekiti Mtaa wa Karume, Kata ya Mnadani ahamasisha usafi