Mwezi wa Maendeleo ya Jamii kujikita kutoa elimu ya Bima ya Afya Dodoma

Na. Mwandishi wetu, DODOMA

Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kuwa na bima ya afya, ikiwa ni sehemu ya shughuli zinazofanyika katika Mwezi wa Maendeleo ya Jamii.


Akizungumza kuhusu elimu hiyo, Mratibu wa Mfuko wa Afya ya Jamii Iliyoboreshwa (iCHF) wa Jiji la Dodoma, Patrick Batimo, alisema kuwa wananchi wanapatiwa elimu kuhusu bima ya afya, ikiwemo Mfuko wa Afya ya Jamii Iliyoboreshwa (iCHF) pamoja na Bima ya Afya kwa Wote.

“Elimu hiyo inalenga kuwawezesha wananchi kuelewa umuhimu wa bima ya afya na namna wanavyoweza kupata huduma za afya kupitia mifumo hiyo”, alisema Batimo.  

Aliongeza kuwa wananchi wanapaswa kutumia fursa ya elimu inayotolewa ili kufahamu aina mbalimbali za bima ya afya, huduma zinazopatikana pamoja na umuhimu wa kuwa na bima wakati wanapohitaji matibabu.

Aidha, utoaji wa elimu hiyo ni sehemu ya juhudi za Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuhakikisha wananchi wanafahamu huduma za bima ya afya na umuhimu wa kujiunga na mifumo hiyo.

Hivyo, wananchi wametakiwa kushiriki katika shughuli za Mwezi wa Maendeleo ya Jamii na kutumia fursa hiyo kupata elimu kuhusu bima ya afya ili kuongeza uelewa na matumizi ya huduma hizo.

Comments

Popular Posts

Kata ya Miyuji Yaongeza Kasi ya Usimamizi Wa Usafi wa Mazingira

Kata za Nkuhungu na Kizota zajiandaa kukabiliana na mvua za El Nino

Zoezi la Kuua Mbwa Wanao Zurura Lafanyika Kata ya Msalato