Barabara za Mtaa wa Mbwanga yafunguliwa, Diwani Kerenge aitaja kuwa chachu ya maendeleo
Na. Mwandishi wetu, Dodoma
Wakazi wa Mtaa wa Mbwanga katika Kata
ya Mnadani wanatarajia kunufaika na usafiri rahisi, kuimarika kwa shughuli za
biashara na kuongezeka kwa fursa za maendeleo kufuatia ufunguzi wa barabara za
mtaa katika uboreshaji wa miundombinu kwa ajili ya maisha bora ya wananchi.
Akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa barabara hiyo, iliyofanyika katika moja ya barabara hizo, Diwani wa Kata ya Mnadani, Mugendi Kerenge alisema kuwa uboreshaji wa miundombinu ya barabara ni nguzo muhimu ya maendeleo kwa kuwa unarahisisha usafirishaji wa watu na bidhaa, kuchochea biashara na kuongeza upatikanaji wa huduma za kijamii.
“Kukamilika kwa barabara zaidi ya
kilomita 14 zimefunguliwa hii ni hatua
muhimu katika safari ya maendeleo ya Kata ya Manadani. Itaondoa changamoto
zilizokuwa zikiwakabili wananchi, hasa wakati wa mvua, na kufungua fursa zaidi
za kiuchumi kwa wakazi wa Mbwanga na maeneo jirani. Natoa shukrani kwa
Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma kwa kutuwezesha kufanikisha hili kwasababu haya ni
baadhai ya mazimio katika Baraza la Madiwani mbapo iliadhimiwa kuwa barabara
zote zifunguliwa na bahati nzuri mtaa wangu wa Mbwanga umekuwa wa kwanza kupata
fursa hii” alisema Kerenge.
Aliwataka wananchi kuzitunza barabara
hizo kwa kuepuka vitendo vinavyoweza kuziharibu, akisisitiza kuwa miundombinu
ya umma ni mali ya wananchi wote na inapaswa kulindwa ili iendelee kutoa huduma
kwa muda mrefu.
Aliongeza kwa kuwahimiza wakazi wa kata hiyo kuendelea kushirikiana na viongozi katika kutekeleza miradi ya maendeleo, akieleza kuwa kwa yeyote anayetaka kununua eneo kufuata taratibu ili kuepuka kuuziwa maeneo yaliyotengwa kwaajili ya barabara.
Kwa upande wake mkazi wa Mtaa wa
Mbwanga, Jamira Rashid aliishukuru serikali kwa kufanikisha ufunguzi wa
barabara hizo, akisema kuwa mradi huo utakuwa chachu ya maendeleo kwa wananchi.
“Barabara hizi ni ukombozi mkubwa kwa
wananchi wetu kwa kuwa zitarahisisha usafiri, biashara na shughuli mbalimbali
za maendeleo hata kama ikitokea dharura kama moto au mgonjwa basi gari litafika
kiurahisi. Pia tunawashukuru wote waliohusika hadi kufikia hatua hii,” alisema
Rashid.
Ufunguzi wa barabara katika Kata ya
Mbwanga ni jambo ambalo litakwenda kuongeza kasi ya maendeleo kwasababu itarahisisha
kupeleka na kufikia mindombinu ya shule, hospitali na maji.
Comments
Post a Comment