Madiwani Dodoma wapongeza ukusanyaji mapato na utekelezaji Bajeti ya 2025/2026

Na. Tutindaga Nkwindi, DODOMA

 

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma limepokea taarifa ya utendaji kazi wa halmashauri kwa mwaka wa Fedha 2025/2026, huku wajumbe wakipongeza juhudi za menejimenti katika ukusanyaji wa mapato na utekelezaji wa bajeti.

 


Akiwasilisha taarifa hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Vincent Odero alisema kuwa juhudi za ukusanyaji wa mapato zimeiwezesha halmashauri kutekeleza mipango na bajeti wake kwa ufanisi.

 

Kwa upande wake Mbunge wa Viti Maalum, Aisha Msantu alisema kuwa menejimenti ya halmashauri imefanya kazi kubwa katika kukusanya mapato na kuhakikisha yanatumika kutekeleza bajeti.

 

“Nawapongeza kwa kazi kubwa ya kukusanya mapato na kuvuka lengo pia mmehakikisha yanatumika ipasavyo kutekeleza bajeti ya halmashauri” alisema Msantu.

 

Nae Diwani wa Kata ya Ihumwa, Edward Magawa ameipongeza menejimenti kwa utekelezaji wa bajeti na kusisitiza umuhimu wa kusimamia vyanzo vya mapato, ikiwemo Soko la Job Ndugai na ‘Lorry Park’, ili viweze kuleta tija na kuchangia maendeleo ya Jiji.

 


Baraza hilo limesisitiza umuhimu wa kuendelea kusimamia vyanzo vya mapato na kuhakikisha mapato yanayokusanywa yanatumika kwa malengo yaliyokusudiwa na kwa manufaa ya wananchi.

Comments

Popular Posts

Kata ya Miyuji Yaongeza Kasi ya Usimamizi Wa Usafi wa Mazingira

Kata za Nkuhungu na Kizota zajiandaa kukabiliana na mvua za El Nino

Mwenyekiti Mtaa wa Karume, Kata ya Mnadani ahamasisha usafi