Wananchi Kata ya Msalato wapongezwa kujitokeza kwa wingi uzinduzi wa Kampeni ya Usafi wa Mazingira Dodoma
Na. Amoni Sambulila, MSALATO
Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri
amewapongeza na kuwashukuru wananchi kwa kujitokeza kwa wingi kushiriki katika
uzinduzi wa Kampeni ya Usafi wa Mazingira mkoani Dodoma, uliofanyika katika
eneo la Mnada wa Msalato, Halmashauri ya Jiji la Dodoma.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo, Alhaj Shekimweri alisema kuwa ushiriki wa wananchi unaonesha umuhimu wa jamii kushirikiana katika kutunza mazingira na kuhakikisha maeneo yanayowazunguka yanakuwa safi na salama.
Aliongeza kwa kuwataka wananchi kuendelea kufanya usafi
katika maeneo yao na kushiriki kikamilifu katika shughuli za usafi ili
kuimarisha afya na ustawi wa jamii.
Kwa upande wake, mwananchi wa Kata ya Msalato, Amani
Merick alisema kuwa kampeni hiyo ni muhimu katika kuhamasisha jamii kuwa na
utamaduni wa kutunza mazingira na kuzingatia usafi katika maeneo wanayoishi na
kufanyia shughuli zao.
Nae, mkazi wa Dodoma, Hadija Yusuf aliwataka wananchi
kuendeleza ushiriki wao katika shughuli za usafi na kuhakikisha mazingira
yanabaki katika hali nzuri kwa manufaa ya jamii.
Usafi wa mazingira ni jukumu la jamii nzima, hivyo
ushiriki wa kila mwananchi ni muhimu katika kuhakikisha maeneo ya makazi,
biashara na maeneo ya umma yanakuwa safi na salama na pia juhudi za kutunza mazingira zinahitaji
ushiriki wa wananchi kwa kuendelea kufanya usafi.
Comments
Post a Comment