Posts

Diwani Kata ya Miyuji azindua kampeni ya usafi wa Mazingira

Image
Na. Mwandishi wetu, MIYUJI   Diwani wa Kata ya Miyuji, Ringo Iringo, amezindua kampeni ya usafi wa mazingira kwa kushirikiana na wataalamu wa Kanda Namba Sita huku akiwataka wananchi kushiriki kikamilifu katika kuhakikisha mazingira yanakuwa safi na salama.   Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo, Iringo amesema kuwa usafi wa mazingira ni jukumu la kila mwananchi na kwamba juhudi za pamoja zinahitajika ili kukabiliana na changamoto ya uchafu katika maeneo ya makazi na maeneo ya wazi.   “Nawasihi wananchi wote tushirikiane katika kuhakikisha mazingira yetu yanakuwa safi. Usafi ni msingi wa afya bora na maendeleo ya jamii,” amesema Iringo.   Amesema kuwa kampeni hiyo inalenga kuhamasisha wananchi kuwa na utamaduni wa kufanya usafi mara kwa mara, kutunza maeneo yao na kuepuka kutupa taka hovyo.   Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Mtaa wa Miyuji Proper, Hawad Mbogela, amewataka wananchi kuunga mkono kampeni hiyo na kuhakikisha usafi unaendelea ...

Kata za Nkuhungu na Kizota zajiandaa kukabiliana na mvua za El Nino

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA   Kanda Namba Tatu ya utoaji huduma katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma imefanya zoezi la usafi wa maeneo ya Kizota Relini na Mkonongo, Kata ya Nkuhungu, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kukabiliana na athari zinazoweza kusababishwa na mvua kubwa za El Niño.   Zoezi hilo lilihusisha ufunguaji na usafishaji wa mitaro, uondoaji wa taka pamoja na ukaguzi wa miundombinu ya kupitisha maji, hatua zinazolenga kupunguza hatari ya maji kujaa katika maeneo ya makazi na biashara.   Kaimu Meneja wa Kanda Namba Tatu, Vestina Manota aliwashukuru watumishi na wananchi kwa kushiriki katika zoezi hilo, akisema usafi wa mazingira ni muhimu katika maandalizi ya kukabiliana na athari za mvua za El Niño.   “Tunawahimiza wananchi kuendelea kufanya usafi kila siku na kuondoa taka kwenye mitaro ili kuhakikisha maji yanapata njia ya kupita kwa urahisi,” alisema Manota.   Diwani wa Kata ya Nkuhungu, Julius Ezekiel aliwataka wananchi kuchukua ta...

Familia 96 kunufaika na mradi wa makazi ya Askari Dodoma

Image
 

Polisi yaokoa fedha na kujenga ghorofa la makazi Dodoma

Image
 

Kituo Kikuu cha Polisi Dodoma kuunganishwa TEHAMA

Image
 

Ujenzi Kituo kipya cha Polisi Dodoma wafikia 61%

Image
 

Kata ya Miyuji Yaongeza Kasi ya Usimamizi Wa Usafi wa Mazingira

Image
Na. Manase Malima, MIYUJI   Kata ya Miyuji katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma imechukua hatua za kuimarisha usafi wa mazingira kwa kufanya ukaguzi wa vikundi vinavyohusika na ukusanyaji na uondoshaji wa taka, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan wa kuhakikisha miji na majiji yanakuwa safi. Katika kutekeleza wito huo, wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan wa kuhakikisha miji na majiji yanakuwa safi, Kata ya Miyuji katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma   imeelekeza nguvu katika kuboresha mfumo wa ukusanyaji na uondoshaji wa taka kupitia vikundi vinavyofanya shughuli hiyo katika mitaa ya kata. Leo tarehe 11 Septemba, 2026 Kamati ya Maendeleo ya Kata ya Miyuji, ikiongozwa na Diwani wa Kata hiyo, Ringo Iringo, imefanya ukaguzi wa vifaa vinavyotumika katika shughuli za usafi, ikiwemo magari, na vifaa kinga kwa watendaji. Ukaguzi huo umehusisha kuangalia hali ya vifaa, mahitaj...

Maadhimisho ya Siku ya Kuzuia Kujitoa Uhai Duniani

Image
 

Match Day Dodoma Jiji FC v Namungo

Image
 

Polisi yaokoa fedha, yaongeza ujenzi wa jengo la ghorofa tatu mradi wa makazi Dodoma

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Jeshi la Polisi Wilaya ya Dodoma limepongezwa kwa kufanikiwa kuokoa fedha katika utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa majengo ya makazi ya askari wa vyeo vya ‘rank and file’ hatua iliyowezesha kuongeza jengo moja la ghorofa tatu licha ya mradi awali kulenga kujenga majengo manane.   Akizungumza wakati wa kukagua maendeleo ya mradi huo eneo la Kutuliza Ghasia Jiji la Dodoma, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri alikipongeza Kikosi Kazi cha Ujenzi cha Jeshi la Polisi kwa kutumia rasilimali zilizopo kwa ufanisi na kuwezesha kuokoa fedha za umma.   Alisema kuwa hatua hiyo ni mfano wa namna taasisi za serikali, hususan vyombo vya ulinzi na usalama, zinavyoweza kutanguliza uzalendo na matumizi bora ya fedha za umma katika kutekeleza miradi ya maendeleo.   “Kwa hili tunawapongeza kwa dhati. ‘Mme-demonstrate’ kama vyombo vya ulinzi na usalama mkipewa majukumu haya ya nchi, mnatanguliza mbele uzalendo na kuokoa fedha za umma. Hili ni...