Wananchi Dodoma Makulu wajitokeza kwa wingi zoezi la usafi wa Mazingira
Na. Amoni Sambulila, DODOMA MAKULU
Wananchi
wa Kata ya Dodoma Makulu wamejitokeza kwa wingi kushiriki katika zoezi la usafi
wa mazingira, ikiwa ni hatua ya kuhamasisha usafi na kuhakikisha mazingira
yanakuwa safi na salama kwa jamii.
Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Msangalale Magharibi, Lucy Michael amewataka wananchi kuendelea kujitoa kwa wingi kufanya usafi na kuhakikisha unafanyika kila siku ili kuepuka magonjwa mbalimbali yanayoweza kusababishwa na uchafu wa mazingira. “Nawasihi wananchi wenzangu kujitokeza kwa wingi katika zoezi la usafi. Pia nasisitiza kuwa usafi wa mazingira ufanyike kila siku kwasababu utatuepusha na magonjwa mbalimbali yanayotokana na uchafu wa mazingira,” alisema Michael.
Kwa
upande wake, Mwananchi Kalleb Wilson alisema kuwa wananchi wanapaswa kuendelea
kushiriki katika zoezi la usafi wa mazingira na kuhakikisha maeneo yao yanakuwa
safi wakati wote.
Nae,
Afisa Biashara Kanda Namba Nne, Johari Fadhili alisema kuwa upo umuhimu mkubwa
kwa wananchi kuendelea kutunza mazingira yao kwa kufanya usafi mara kwa mara
ikiwemo kuepuka magonjwa pamoja na faini zinazoweza kutolewa kutokana na
kutokufanya usafi.
Zoezi
la usafi limefanyika katika Kata ya Dodoma Makulu, huku wananchi wakihimizwa
kuendeleza utamaduni wa kufanya usafi kila siku kwa ajili ya kulinda afya na
mazingira ya jamii na kuliweka jiji safi.
Comments
Post a Comment