Polisi yaokoa fedha, yaongeza ujenzi wa jengo la ghorofa tatu mradi wa makazi Dodoma
Na. Mwandishi wetu, DODOMA
Jeshi la Polisi Wilaya ya Dodoma limepongezwa kwa kufanikiwa kuokoa fedha katika utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa majengo ya makazi ya askari wa vyeo vya ‘rank and file’ hatua iliyowezesha kuongeza jengo moja la ghorofa tatu licha ya mradi awali kulenga kujenga majengo manane.
Alisema
kuwa hatua hiyo ni mfano wa namna taasisi za serikali, hususan vyombo vya
ulinzi na usalama, zinavyoweza kutanguliza uzalendo na matumizi bora ya fedha
za umma katika kutekeleza miradi ya maendeleo.
“Kwa
hili tunawapongeza kwa dhati. ‘Mme-demonstrate’ kama vyombo vya ulinzi na
usalama mkipewa majukumu haya ya nchi, mnatanguliza mbele uzalendo na kuokoa
fedha za umma. Hili ni jambo la mfano. Lakini hata kabla ya kupokea zile fedha
zote, tayari mmeweza kufanya ‘savings’ na mnaongeza jengo lingine la ziada
katika mradi huu,” alisema Alhaj Shekimweri.
Akitoa
maelezo ya mradi huo, Mhandisi wa Polisi, ASP Gaston Nombo, alisema kuwa awali
mradi uliwasilisha andiko la kuomba shilingi bilioni 18.96 lakini hadi sasa
shilingi bilioni 16.78 zimepokelewa, huku sehemu ya fedha hizo ikiokolewa na
kuwezesha kuanza ujenzi wa jengo moja na kufikisha jumla ya majengo tisa.
Alisema
kuwa wameongeza pia ujenzi wa uzio wa takribani kilomita 1.4 kuzunguka kambi
hiyo, ambao unaendelea kwa hatua mbalimbali, ikiwamo ujenzi wa tofali, upakaji
wa plasta na ‘capping’.
“Na
mradi huu kabla ya ‘variation’ ya bei, jengo moja lilikuwa linagharimu bilioni
2.03. Sasa hivi limeongezeka linaenda na bilioni 2.37. Na andiko lilikuwa
tupate bilioni 18. So far tumepata bilioni 16.7, ambazo pia tume-save, tumeanza
kujenga ghorofa la tisa,” alisema ASP Nombo.
Mradi
huo unaendelea kutekelezwa kwa kutumia nguvu kazi ya ndani, huku fedha
zilizookolewa zikielekezwa katika kuongeza thamani ya mradi kwa kuanza ujenzi
wa jengo la tisa na uzio wa kilomita 1.4, hatua inayolenga kuboresha mazingira
ya makazi na usalama wa askari pamoja na familia zao.
MWISHO
Comments
Post a Comment