Huduma ya Maji kuimarika Dodoma
Na. Dennis Gondwe, DODOMA
HALI ya upatikanaji wa huduma ya Maji safi na salama
imeendelea kuimarika hadi kufikia lita 88.7 kwa siku sawa na asilimia 55 ya mahitaji
yote.
Kauli ilitolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi alipokuwa akisoma Risala ya Utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma katika uwanja wa Shule ya Msingi Kizota jijini Dodoma.
Alisema kuwa hali ya
upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama ni lita Mil. 88.7 kwa siku sawa na
asilimia 55 ya mahitaji ya wakazi wote ambayo ni lita Mil. 159.9. DUWASA
imeendelea kutekeleza miradi 38 ya shilingi bilioni 91. ambayo ikikamilika
itaongeza upatikanaji wa Maji kwa zaidi ya asilimia 75 ya mahitaji ya siku.
MWISHO
Comments
Post a Comment