Dodoma kupambana na VVU

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

WILAYA ya Dodoma imeendelea kupambana na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI (VVU) ikiwa na maambukizi ya asilimia 2.7 kwa Mwaka 2025.



Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi alipokuwa akisoma Risala ya Utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma katika uwanja wa Shule ya Msingi Kizota jijini Dodoma.

Alisema kuwa mapambano dhidi ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI yanapewa uzito mkubwa. ”Mheshimiwa Rais, hali ya ushamiri wa maambukizi ya VVU wilayani kwa mwaka 2025 ni asilimia 2.7. Aidha, chini ya Kaulimbiu inayosema “Imarisha mwitikio; Tokomeza UKIMWI”, kwa kipindi cha Januari, 2025 hadi Desemba, 2025 jumla ya watu 89,562 (Me 34,806 Ke 54,756) walijitokeza kupima maambukizi ya Virusi vya UKIMWI kwa hiari, kati yao watu 2,432 walikutwa na maambukizi na kuunganishwa na huduma za tiba na matunzo kwa WAVIU.  Hata hivyo, katika kuhakikisha tunafikia lengo la kitaifa la 95-95-95 ifikapo mwaka 2030, hadi kufikia Aprili, 2026 asilimia 96.3 ya watu wanaoishi na maambukizi ya VVU walitambua hali zao na kati yao asilimia 97.7 wanatumia dawa za kufubaza virusi vya UKIMWI na asilimia 95.6 wamefanikiwa kufubaza chini ya nakala 1,000. Aidha, elimu imeendelea kutolewa kwa jamii kwa njia ya redio na warsha ili kudhibiti maambukizi mapya” alisema Mbugi.

Mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI yanaongozwa na kaulimbiu inayosema “Imarisha mwitikio; Tokomeza UKIMWI”.

MWISHO

 

Comments

Popular Posts

Wilaya ya Dodoma yapata “clean sheet” Miradi ya Mwenge wa Uhuru 2026