Dodoma Jiji FC yawaalika mashabiki kujitokeza kwa wingi dhidi ya Namungo
Na. Amoni Sambulila, DODOMA
Timu ya Dodoma Jiji FC imewaalika mashabiki wa klabu
hiyo kujitokeza kwa wingi katika mchezo dhidi ya Timu ya Namungo utakaofanyika leo
Ijumaa majira ya saa moja usiku katika Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kuelekea mchezo huo, Msemaji wa Timu ya Dodoma Jiji FC, Moses Mpunga amewataka mashabiki kujitokeza kwa wingi uwanjani na kuendelea kuipa timu yao sapoti katika mchezo huo.
“Uwepo wa mashabiki kwa wingi uwanjani ni muhimu kwa
timu yetu, kwasababu sapoti yao inaweza kuongeza morali na kuipa nguvu Timu ya Dodoma
Jiji FC katika kipindi chote cha mchezo” amesema Mpunga.
Aliongeza kuwa wanatambua mchango wa mashabiki katika
kuisapoti timu na hivyo kuwaomba waendelee kujitokeza katika michezo ya timu
hiyo, hasa katika mchezo huo dhidi ya Namungo.
MWISHO
Comments
Post a Comment