Miundombinu ya elimu kuing’arisha Msembeta S/M

Na. Jesca Kipingu, DODOMA


Mradi wa umaliziaji wa ujenzi wa matundu 13 ya vyoo katika Shule ya Msingi Msembeta, umefikia asilimia 90 ya utekelezaji, ambapo kazi mbalimbali za ujenzi na umaliziaji wa miundombinu hiyo zinaendelea kwa kasi kuelekea kukamilika kwake.



Mradi huo unatekelezwa kwa gharama ya shilingi 38,905,912.75, fedha zinazotokana na mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Sambamba na hilo, halmashauri imefanikiwa kukamilisha kwa asilimia 100 mradi wa umaliziaji wa nyumba moja ya mwalimu katika Shule ya Msingi Msembeta. Mradi huo umegharimu jumla ya shilingi 40,100,000, fedha ambazo pia zimetolewa kupitia mapato ya ndani ya halmashauri.

Kukamilika kwa miradi hii kunatarajiwa kuleta nafuu kwa walimu na wanafunzi, huku kukiwa na ongezeko la mazingira bora ya ufundishaji na ujifunzaji. Uwekezaji huo unaendelea kuonesha dhamira ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika kuimarisha sekta ya elimu kwa kutambua kuwa miundombinu bora ni msingi muhimu wa utoaji wa elimu yenye ubora.

Halmashauri ya Jiji la Dodoma inaendelea kuelekeza miradi yenye manufaa kwa wananchi kupitia mapato ya ndani, kwa lengo la kuhakikisha maendeleo yanafika katika maeneo mbalimbali na kuboresha huduma muhimu za kijamii.

 

#Mapato ya Ndani kwa Maendeleo ya Dodoma Jiji.

#DodomaJiji #MapatoYaNdani #Elimu #Msembeta #MiradiYaMaendeleo #MiundombinuYaElimu

Comments

Popular Posts

Vijana watakiwa kujiendeleza nje ya mfumo rasmi

NGOs zatakiwa kuzingatia uwazi na uwajibikaji Dodoma