Wataalam Ilemela MC wajifunza mfumo wa utenganishaji taka Dodoma Jiji
Wataalam
kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela wamefanya ziara ya mafunzo ya mbinu
bora za usimamizi wa usafi wa mazingira hasa mfumo wa kutenganisha taka na
kuona vihifadhio vinavyotumika kutenganishia taka katika Halmashauri ya Jiji la
Dodoma.
Ziara
hiyo ya mafunzo ilijifunza jinsi kampuni maalum ya kutekeleza miradi (SPV) ya
halmashauri inavyotumika kutekeleza miradi ya maendeleo na kutembelea miradi
inayotekelezwa ya Bustani ya Mapumziko ya Chinangali na Duka kuuza vifaa vya ujenzi.
Comments
Post a Comment